中国国际广播电台
Katika
historia ya kale ya China
migogoro kati ya kabila la
Wahan na makabila mengine
ikitokea, ilikuwa inatatuliwa
kwa vita, lakini pia iliwahi
kutokea njia nyingine ya kutatua
migogoro kati ya makabila,
nayo ni kumwoza binti wa mfalme
kwenye kabila jingine na kupata
urafiki na kabila hilo.
Karne ya kwanza ilikuwa ni
kipindi cha Enzi ya Han. Kabila
la Waxiongnu lililokuwa katika
sehemu ya kusini magharibi
ya China lilikumbwa na migogoro
kutokana na watemi kugombea
madaraka. Wakati huo mtemi
mmoja aliyejulikana kwa jina
la Han Xie alikuja kwa mfalme
wa Enzi ya Han kuomba msaada.
Mfalme wa Enzi ya Han alimkaribisha
kwa ukarimu na alimsaidia
kwa nafaka nyingi, na baada
ya kurudi alifanikiwa kupata
utawala wa kabila la Waxiongnu.
Ili kupata urafiki wa daima
mwaka 33 K.K. Han Xie kwa
mara nyingine alikuja mji
mkuu kuonana na mfalme na
kuomba amwoe binti yake. Mfalme
wa Enzi ya Han mara alikubali
ombi lake. Mfalme aliwaambia
vijakazi wake “kati yenu atakayekubali
kuwa mke wa mfalme wa kabila
la Xiongnu atakuwa binti yangu.”
Kulikuwa na msichana mmoja
mwenye sura nzuri na werevu,
aliitwa Wang Zhaojun. Msichana
huyo alikuwa mwerevu na kupenda
kusoma, aliweza kutunga mashairi
na kupiga kinanda, alikubali
kuolewa na mfalme wa kabila
la Waxiongnu kwa ajili ya
urafiki wa makabila mawili.
Kwa kusindikizwa na maofisa
wa Enzi ya Han Wang Zhaojun
alisafiri mbali na kufika
sehemu ya kabila la Waxiongnu.
Mwanzoni maisha ya kabila
hilo yalikuwa magumu kwake
lakini baada ya muda alizoea
na kuishi vema na Waxiongnu.
|