中国国际广播电台
Katika kitabu maarufu cha
“Rekodi ya Historia” kilichoandikwa
na Simaqian, walielezwa wanadiplomasia
kadhaa mashuhuri, mmoja wao
alikuwa Yan Zi aliyeishi katika
karne ya sita.
Kipindi kati ya mwaka 770
K.K. hadi 481 K.K. katika
historia ya China kinaitwa
kipindi cha Spring na Autumn.
Wakati huo utawala wa Enzi
ya Zhou ulikuwa umeanza kudhoofika,
madola yaliyo chini ya himaya
kake aylikuwa yanapigana kugombea
ardhi na mwishowe yalitokea
madola kadhaa yenye nguvu
kubwa, na pia walitokea wanasiasa
mashuhuri. Yan Zi alikukwa
mmojawapo.
Kwa mujibu wa maandishi ya
historia, kimo cha Yan Zi
kilikuwa mita moja na sentimita
arobaini tu, lakini elimu
yake ilikuwa pana na alikukwa
mtu mwerevu na mcheshi.
Yan Zi aliwahi kwenda kwenye
madola mengine mara nyingi
akiwa mjumbe wa Dola la Qi,
kati ya safari zake, hadithi
katika safari mbili alipokuwa
katika Dola la Chu zilikuwa
maarufu. Mfalme wa Dola la
Chu alijua yeye ni mbilikimo,
alitaka kumdhihaki. Katika
safari ya kwanza alipokuwa
kwenye Dola la Chu mfalme
aliamuru watu wake wamwingize
mjini kutoka kwenye kilango
kidogo pembeni mwa lango kubwa.
Yan Zi alielewa mfalme Chu
akitaka kumdhalilisha, alikataa
kabisa na kusema, “Nikifika
kwenye dola la mbwa nitaingia
kwenye kilango cha mbwa, sasa
nimekuja kwenye dola la Chu
nikiwa mjumbe wa dola, niwezaje
kuingia mjini kupitia kilango
cha mbwa!” Walinzi walikuwa
hawana budi ila kumpitisha
kutoka kwneye mlango mkubwa.
Mfalme wa Chu alipokutana
na Yan Zi alimwuliza kwa makusudi:
“Kwani dola la Qi linashindwa
kumchagua mtu mwingine aje
kwenye dola la Chu badala
yako?” Yan Zi alimjibu kwa
utaratibu, “Dola la Qi lina
mazoea ya kutuma wajumbe wenye
maadili mema kwenye madola
yenye maadili mema, na kutuma
wajumbe wapumbavu kwenye madola
ya wapumbavu. Mimi ni mpumbavu
kabisa kati ya wajumbe wote,
ndio maana nimetumwa hapa.”
Safari ya pili alipokwenda
kwenye dola la Chu, mfalme
wa Chu alitaka kumwaibisha
Yan Zi hadharani. Wakati mfalme
wa Chu alipomkaribisha kwenye
chakula, ghafla askari wawili
walileta mtu mmoja aliyefungwa
kamba mbele ya mfalme, wakisema
mtu huyo ni mtu wa dola la
Qi, aliiba mali yao. Mfalme
alimtupia macho Yan Zi akisema,
“Kwani watu wa dola la Qi
walizaliwa na wezi?” Mwerevu
Yan Zi mara alikumbuka mto
Huaihe uliokuwa mpaka wa madola
mawili, alitumia michungwa
kumjibu mfalme: “Machungwa
yaliyopatikana kwenye ukingo
wa kusini wa mto ni matamu,
lakini yaliyoko kwenye ukingo
wa kaskazini ni machungu,
sababu udongo wenyewe ni tofauti.
Watu wanaoishi katika dola
la Qi hawaibi, lakini wanaoishi
katika dola la Chu wana tabia
ya kuiba, kwani ardhi ya Chu
inalea wizi?”
Mambo kama hayo yalikuwa
mengi ambayo Yan Zi aliwashinda
wapinzani wake waliojaribu
kumdhihaki na kuharibu heshima
ya dola lake. Alikuwa mwanadiplomasia
mashuhuri katika hitoria ya
China.
|