Guan Zhong na Bao Shuya
中国国际广播电台


     
Guan Zhong na Bao Shuya walikuwa wanasiasa katika karne ya saba na walikuwa marafiki. Guan Zhong alikuwa maskini na Bao Shuya alikuwa tajiri, na hao wawili walifahamiana na kuamiana na hata walishirikiana kufanya biashara, kutokana na umaskini Guan Zhong alitoa raslimali chache, lakini walipogawana faida alipewa pesa nyingi zaidi kuliko Bao Shuya ili aweze kuwatunza jamaa zake.

Baadaye watu hao wawili wote walishiriki katika mambo ya siasa, ambayo wote wawili waliwafundisha watoto wawili wa mfalme wa Dola la Qi katika madola mengine tofauti. Baadaye uasi ulitokea katika Dola la Qi, mfalme aliuawa. Baada ya kusikia habari kuhusu kifo cha baba yao, watoto wote wawili walikimbilia nyumbani dola la Qi ili kurithi kiti cha ufalme. Njiani mtoto Qi Huan Gong na ndugu yake walikutana. Guan Zhong alimfyatulia mshale Qi Huan Gong ili ndugu wa Qi Huan Gong apate nafasi ya ufalme. Mshale huo ulimkwaruza tu Qi Huan Gong kiunoni, lakini alijidai kuwa amepigwa na kuanguka kama amekufa. Ndugu yake alidhani amekwisha kufa, na kiti cha utawala hakika kitakuwa chake, akapunguza mwendo wa safari. Lakini Qi Huan Gong hakuumia, aliharakisha safari yake usiku na mchana na alifika nchini mapema kwa siku sita kuliko ndugu yake, mawaziri walimwunga mkono awe mtawala wa dola la Qi.

Baada ya kuwa mfalme wa dola la Qi, Qi Huan Gong aliwapokea watu wengi wenye busara hata hakuwa na kinyongo na yule Guan Zhong aliyemfyatulia mshale na kumteua kuwa waziri wa dola lake.

Guan Zhong alikuwa waziri kwa miaka mingi na alitoa mchango mkubwa kwa ajili ya kuimarisha dola lake.

Bao Shuya alipofariki, Guan Zhong alilia sana mbele ya kaburi lake, alisema, “nilizaliwa na mama yangu lakini aliyenielewa ni Bao Shuya!”