Mfalme Chu Zhuangwang
中国国际广播电台


      
China ni nchi yenye uvumilivu mkubwa, watu wanaona kuwa uvumilivu unaweza kuyeyusha fitina. Hadithi ya “kuondoa kishungi kwenye kofia” inawafundisha watu wenye uvumilivu watalipwa mema.

Katika kipindi cha Spring na Autumn, karne ya saba, kulikuwa na madola mengi kwa wakati mmoja. Mfalme wa Dola la Chu, Chu Zhuangwang alikuwa mwerevu, na chini ya utawala wake dola hilo liliimarika sana.

Siku moja, mfalme Chu Zhuangwang aliwakaribisha maofisa kwenye chakula na kuburudika kwa nyimbo na ngoma. Giza lilikuwa linaingia, mfalme aliwaambia kuwasha mishumaa. Watu walikula na kunywa kwa furaha.

Ghafla upepo ulivuma, mishumaa ilizimika, wakati huo mke wa mfalme alisikia kuna mkono mmoja ulimshika shika, mke wa mfalme alighadhabika akang’oa kishungi cha kofia ya yule aliyemtomasa, akaenda kwa mfalme na kumnong’oneza, “washa mishumaa na kuona kama nani alikosa kishungi kwenye kufia na kumwadhibu.” Lakini mfalme alipaaza sauti na kusema, “Msiwashe mishumaa, ni furaha pekee kunywa pombe gizani.” Baadaye mfalme aliwauliza maofisa, “Mnafurahia chakula?” wote walijibu “Ndio!” Mfalme aliendelea, “kama kweli mnafurahia chakula, basi ng’oeni vishungi kwenye kofia zenu!” wote waling’oa. Kisha mfalme aliwaambia wawashe mishumaa. Maofisa walipoona kofia zote zilibadilika sura wote walicheka, waliendelea kula na kunywa mpaka kupambazuka.

Baada ya kurudi kwenye kasri la kifalme, mke wa mfalme alihasirika sana alisema, “Wewe mfalme unawadekeza sana maofisa, hivyo utashindwa kuwatawala.” Mfalme alicheka na kusema, “Nawakaribisha maofisa kwenye chakula kwa lengo la kuwafurahisha. Ni jambo la kawaida kwa mtu akizidiwa na pombe na kufanya kitendo kisicho cha kawaida. Nikimwadhibu ofisa huyo kwa jambo hilo dogo nitaharibu furaha na kuwafedhehesha maofisa. Hilo silo lengo la kuwaandalia chakula.”

Baadaye dola la Chu lilishambulia dola la Zheng. Kulikuwa na jemadari mmoja aliyekuwa shupavu mkubwa katika mapambano dhidi ya askari wa dola la Chu, na alifanya mashambulizi mpaka karibu na mji mkuu wa dola la Chu. Jemadari huyo ndiye aliyemshikashika mke wa mfalme wa dola la Chu.

Hadithi ya “kuondoa kishungi kofiani” inawaambia watu wawe wavumilivu.