中国国际广播电台
Katika
mlima wa Yu Shan mkoani Fujian
kuna hekalu moja lililowekwa
sanamu ya Qi Jiguang, watalii
wanapofika huko hawakosi kwenda
kutoa heshima kwake kutokana
na uzalendo wake na mchango
wake katika mapambano dhidi
ya wavamizi.
Qi Jiguang alikuwa jemadari
katika Enzi ya Ming, alizaliwa
katika ukoo wa jemadari. Kwa
kuathiriwa na baba yake, Qi
Jiguang toka alipokuwa mtoto
alipenda sana mambo ya kijeshi
na kuwa na nia ya kuwa mwanajeshi
hodari. Wakati huo wavamizi
wa Japan walikuwa mara kwa
mara wanashambulia China.
Alipokuwa na umri wa miaka
17 alirithi wadhifa wa baba
yake na kuanza maisha yake
ya kijeshi. Alipokuwa tu jemadari
tatizo lililomkabili lilikuwa
ni mashambulizi ya Japan.
Tokea mwishoni mwa Enzi ya
Yuan na mwanzoni mwa Enzi
ya Ming maharamia wa Japan
mara kwa mara walikuwa wakipora
mali na kuua watu kwenye mwambao.
Katika nusu ya pili ya karne
ya 15 maharamia wa Japan walikuwa
wanashirikiana na wafanyabiashara
wabaya wa China kufanya uovu.
Mwaka 1555 Qi Jiguang alitumwa
kwenye mwambao, aliunda jeshi
la wakulima na wachimba migodi.
Walitumia mishale na mikuki
kuwaua baada ya kuwatega mitegoni.
Jeshi lake lilikuwa na askari
elfu 4, na baada ya kuwafundisha
na kuwafahamisha askari mbinu
za kivita, jeshi hilo lilikuwa
hodari sana, na kutokana na
kuwa na nidhamu kali liliungwa
mkono na wananchi.
Mwaka 1561 maharamia wa Japan
elfu kadhaa na mashua zaidi
ya mia walifanya mashambulizi
katika sehemu ya Taizhou mkoani
Zhejiang. Qi Jiguang kwa haraka
aliwaongoza askari wake kupambana
nao na kuwaangamiza maharamia
wote.
Kutokana na juhudi za Qi
Jiguang na majemadari wengine,
maharamia wa Japan walitoweka,
mikoa ya Zhejiang na Fujian
ilikuwa tulivu, na uchumi
ulistawi. Qi Jiguang alitoa
mchango mkubwa katika mapambano
dhidi ya maharamia wa Japan
na alisifiwa sana na watu
wa China.
|