Masimulizi kuhusu Mungu wa Jiko
中国国际广播电台

      Katika miaka zaidi ya elfu mbili, Wachina wamekuwa na mila ya kufanya tambiko kwa mungu wa jiko katika tarehe 23 mwezi Februari kwa kalenda ya Kichina.

Mungu wa Jiko alitokea katika hadithi za mapokeo, yeye ni ofisa aliyetumwa na mungu kwenye kila familia, na kila mwaka anakwenda kwa mungu kutoa ripoti. Kwa hiyo watu humwabudu sana na kwa ajili ya kumfurahisha, kila mwaka katika siku hiyo watu hufanya tambiko.

Zamani za kale kulikuwa na tajiri mmoja aliyeitwa Zhang Sheng, mke wake Ding Xiang alikuwa kisura na mwenye akili. Mwanzoni waliishi kwa furaha sana.

Siku moja tajiri huyo alimkuta msichana mmoja mrembo aliyeitwa Hai Tang, mara walianza kupendana. Muda si mrefu baadaye tajiri alimwoa na kumleta nyumbani. Msichana Hai Tang alipoona mke wa tajiri alikuwa mrembo na ni mke halali alikuwa na wivu, alimtaka tajiri kumfukuza.

Tokea hapo Zhang Sheng na mkewe waliishi maisha ya anasa, na kabla ya kutimia miaka miwili, walifuja mali zote na wote walikuwa maskini. Kwa kuona kuwa Zhang Sheng amekuwa maskini, Hai Tang alimwacha na kuolewa na mwengine. Zhang Sheng alibaki peke yake, kwa kulazimika na umaskini alibadilika kuwa ombaomba. Siku moja theluji ilikuwa kubwa, Zhang Sheng alisikia baridi na njaa, alianguka mbele ya mlango wa nyumba ya tajiri mmoja. Mtumishi alipotoka nyumbani alimwona na kumsaidia kumpeleka jikoni. Dakika chache baadaye mwenye nyumba alikuja kumwangalia, Zhang Sheng alishtuka alipofahamu kuwa huyo mwenye nyumba ndiye aliyekuwa mkewe Ding Xiang. Kwa kuona aibu alijipenyeza ndani ya tundu la kijiko cha kuwashia kuni. Ding Xiang alipoingia jikoni hakumwona yeyote, aliona ajabu, kisha baadaye aligundua kitu fulani kilichoziba tundu la kijiko, alikivuta kitu hicho akatambua ni mtu aliyekuwa mumewe ambaye amekwisha kufa kutokana na kuungua na moto. Siku chache baadaye Ding Xiang alikufa kutokana na huzuni. Mungu alipopata habari hiyo aliona kuwa Zhang Sheng ni mtu mwema, alijuta makosa yake, alimteua kuwa mungu wa jiko. Watu walimwabudu mungu huyo wa jiko na mkewe pia, na kuweka sanamu zao ndani ya jiko.

Ili mungu awasemee wema mbele ya mungu, watu hupika sukari ya kimea iliyonatanata kwa nafaka, ili mungu wa jiko anapokula sukari hiyo ulimi utakuwa ladha tamu na kusema maneno mazuri juu ya familia aliyokaa.