Vyakula vya Aina Tatu katika Sikukuu Tatu
中国国际广播电台

      Nchini China kuna sikukuu tatu kubwa, nazo ni sikukuu ya taa, sikukuu ya mashindano ya mbio za mashua ya dragoni na sikukuu ya mwezi kwa kalenda ya Kichina. Katika sikukuu hizo tatu kuna vyakula maalumu.

Tahere 15 ya mwezi wa Januari kwa kalenda ya Kichina ni sikukuu ya taa. Katika siku hiyo watu wa China wana mila ya kula vidonge vitamu vya unga unaonata, Wachina wa sehemu ya kaskazini wanaviita vidonge hivyo kwa jina la Yuanxiao , na watu wa sehemu ya kusini wanaita kwa jina la Tangyuan , na namna za kutengeneza zinatofautiana.

Katika sehemu ya kaskazini ya China vidonge hivyo hutengenezwa kwa unga wa mchele unaonata, na ndani ya vidonge hutiwa vijazo vya sukari, simsim, karanga iliyosagwa. Kila sikukuu hiyo inapokaribia vidonge hutayarishwa madukani,

Katika sehemu ya kusini ya China watu hutengeneza vidonge vidogo vidogo na kutia vijazo vyenye chembe za karanga, simsim, unga wa tende na kunde nyekundu.

Vidonge hivyo huchemshwa, ni laini na ni vitamu, ikimaanisha kuungana kwa jamaa.

Sikukuu ya mashindano ya mbio za mashua ya dragoni iko katika tarehe tano mwezi wa tano kwa kalenda ya Kichina. Katika siku hiyo Wachina wana mila ya kula Zongzi , chakula ambacho mchele unaonata pamoja na tende hufungwa kwa majani ya matete kama sambusa na kuchemshwa. Vijazo ndani ya Zongzi huwa tofauti kati ya sehemu ya kaskazini na kusini.

Masimulizi ya mapokeo yanasema kuwa watu wana mila ya kula Zongzi ili kumkumbuka mshairi mkubwa Qu Yuan. Karne ya tatu dola la Chu aliloishi Qu Yuan lilitekwa, kutokana na huzuni na hasira Qu Yuan alijitupa ndani ya mto tarehe 5 mwezi wa tano kwa kalenda ya Kichina. Watu wa wanaofuata walianza kutengeneza Zongzi na kutupa mtoni kumfanyia tambiko.

Zongzi ni chakula na pia ni zawadi kwa marafiki na jamaa. Katika siku hiyo marafiki na jamaa hutembeleana na kupeana Zongzi .

Tarehe 15 Agosti kwa kalenda ya Kichina ni sikukuu ya mwezi, kwa sababu katika siku hiyo mwezi ni mviringo na unang'ara kabisa katika mwaka mzima. Watu huburudika kwa mwezi wakati usiku na huku wakila keki za duara mithili ya mwezi. Ndani ya keki hutiwa vijazo vya aina tofauti.

Keki hutengenezwa kwa duara mithili ya mwezi mviringo. Katika siku za kale watu walikuwa wanaandalia keki hizo uani na kuabudu mwezi. Baada ya ibada wanakula keki hizo. na siku hiyo pia ina maana ya kujumuika kwa jamaa wanaoishi katika sehemu tofauti, wanakula pamoja katika usiku huo wenye mwezi mpevu.

Keki za mwezi hupikwa kwa ladha tofauti kutokana na sehemu tofautu nchini China.

Kufuatana na jinsi maisha yanavyokuwa bora keki hupikwa kwa vijazo vilivyo bora zaidi, kuna vijazo vya sukari, unga wa tende, unga wa kunde nyekundu, nyama, kiini cha yai la bata, vipande vya matunda na krimu.

Keki za mwezi pia ni zawadi kwa jamaa na marafiki. Katika siku za kabla ya sikukuu hiyo keki za mwezi hujaa madukani.