中国国际广播电台
Mfumo wa nchi
Jamhuri ya Watu wa China ni
nchi ya ujamaa ya utawala
wa kidemokrasi ya umma chini
ya uongozi wa tabaka la wafanyakazi
na kwenye msingi wa shirikisho
la wafanyakazi na wakulima.
Mfumo wa ujamaa ni mfumo wa
kimsingi wa Jamhuri ya watu
wa China.
Katiba
Katiba ni sheria kuu ya kimsingi
ya taifa, ambayo huamua mfumo
wa jamii wa nchi na kanuni
za kimsingi za mfumo wa nchi,
kanuni za kimsingi za jumuia
na shughuli za idara za serikali,
haki za kimsingi na majukumu
ya raia, katiba pia inaamua
bendera ya taifa, wimbo wa
taifa, nembo ya taifa na mji
mkuu pamoja na taratibu muhimu
nyingine ambazo zinahusiana
na pande zote za maisha ya
nchi. Katiba ina madaraka
makubwa ya sheria ambayo ni
msingi wa sheria nyingi, sheria
zote na kanuni zote haziruhusiwi
kwenda kinyume na katiba.
“Mwongozo wa pamoja wa Baraza
la mashauriano ya kisiasa
la umma la China” uliotangazwa
kabla ya kuanzishwa kwa Jamhuri
ya watu wa China, si kama
tu ni mwongozo wa muungano
wa demokrasia ya umma wa China,
bali pia unaonesha umuhimu
wa katiba ya muda. “Mwongozo
wa pamoja” ulipitishwa kwenye
mkutano wa kwanza wa Baraza
la mashauriano ya kisiasa
la umma la China, ambao ulitangazwa
tarehe 29 Septemba mwaka 1949.
Kabla ya kutangazwa kwa “Katiba
ya Jamhuri ya watu wa China”,
mwongozo huo ulifanya kazi
ya katiba ya muda.
Baada ya kuanzishwa kwa Jamhuri
ya watu wa China tarehe 1
Oktoba, 1949, katiba nne za
Jamhuri ya watu wa China zilitungwa
na kutangazwa mwaka 1954,
mwaka 1975, mwaka 1978 na
mwaka 1982.
Katiba ya 4 ya China yaani
katiba ya sasa ilitangazwa
tarehe 4 Desemba, 1982 kwenye
Mkutano wa 5 wa Bunge la 5
la umma la China. Katiba hiyo
ilirithi na kuendeleza kanuni
za kimsingi za katiba iliyotangazwa
mwaka 1954, kujumuisha maarifa
ya China ya maendeleo ya ujamaa
na kuigiza maarifa ya kimataifa,
ambayo ni sheria kuu ya kimsingi
yenye umaalum wa kichina inayolingana
na mahitaji ya ujenzi wa mambo
ya kisasa ya ujamaa. Katiba
hiyo imeweka bayana mifumo
ya kisiasa na kiuchumi ya
Jamhuri ya watu wa China,
haki na majukumu ya raia,
kuanzishwa kwa wizara za nchi
na kazi za wizara hizo na
majukumu ya kimsingi ya nchi
ya siku zijazo. Umaalum wake
wa kimsingi ni kuweka mfumo
wa kimsingi na majukumu ya
kimsingi ya China, kuthibitisha
kanuni nne za kimsingi na
sera ya kimsingi ya mageuzi
na ufunguaji mlango. Katiba
hiyo inaeleza kuwa, wananchi
wa makabila mbalimbali na
jumuiya zote za taifa zima
yapaswa kuchukua katiba kuwa
kanuni za kimsingi za shughuli
zao, na jumuiya yoyote au
mtu yeyote haruhusiwi kuwa
na haki maalum zinazokiuka
katiba na sheria.
Katiba hiyo inagawanyika kuwa
sehemu tano za mwongozo wa
jumla, haki za kimsingi na
majukumu ya raia, wizara za
nchi, bendera ya taifa, nembo
ya taifa, na mji mkuu wa China,
katiba hiyo ina milango minne
na vifungu 138 kwa jumla.
Tangu kutangazwa kwake, China
ilifanya marekebisho manne
kuhusu katiba hiyo ili kuikamilisha
siku hadi siku.
Mfumo wa Bunge la
umma la China
Mfumo wa Bunge la umma la
China ni mfumo wa siasa wa
kimsingi, ambao ni aina ya
jumuiya ya utawala wa kidemokrasia
wa umma wa China, pia ni mfumo
wa siasa wa China. Bunge la
umma la China ni tofauti na
mabunge ya nchi za magharibi
chini ya “nguzo tatu za utawala”,
bunge la umma la China limethibitishwa
kwenye katiba ya China kuwa
chombo chenye madaraka ya
juu kabisa cha taifa. Kila
raia mwenye umri wa zaidi
ya miaka 18 ana haki ya kuchagua
mjumbe wa bunge la umma au
kuchaguliwa kuwa mjumbe wa
bunge la umma. Nchini China,
katika bunge la umma kwenye
ngazi tofauti, wajumbe wa
bunge la umma la ngazi ya
tarafa na wilaya huchaguliwa
moja kwa moja. Wajumbe wa
ngazi juu ya tarafa na wilaya
wanachaguliwa kwa njia isiyo
ya moja kwa moja. Bunge la
umma la China linaundwa na
wajumbe wanaochaguliwa kutoka
mikoa, mikoa inayojiendesha,
miji inayotawaliwa moja kwa
moja na serikali kuu na jeshi.
Muda wa kila awamu ya Bunge
la umma la China kwenye ngazi
mbalimbali ni miaka mitano,
na kila bunge la China hukutana
mara moja
Kwenye mkutano wa mwaka wa
Bunge la umma la China, wajumbe
wa bunge la umma wanasikiliza
ripoti ya kazi ya serikali
na ripoti nyingine muhimu
kadhaa, wanatakiwa kuthibitisha
ripoti hizo na kutoa maazimio
husika. Katika kipindi cha
kufungwa kwa mkutano wa bunge
la umma, Halmashauri ya kudumu
ya bunge la umma la ngazi
mbalimbali inaendesha madaraka
inayokabidhiwa kutoka kwa
bunge la umma. Kwa mfano,
madaraka ya Halmashauri ya
kudumu ya Bunge la umma la
China ni pamoja na kufafanua
katiba, kusimamia utekelezaji
wa katiba, kutunga na kurekebisha
sheria zilizoko nje ya sheria
zilizotungwa na bunge la umma,
kuwajibika kwa bunge la umma
la taifa na kutoa ripoti za
kazi.
Madaraka ya kimsingi ya Bunge
la umma la China ni pamoja
na kutunga sheria, kufanya
usimamizi, kutoa maamuzi kuhusu
mambo makubwa na kuwateua
viongozi au kuwaondoa viongozi
madarakani. Nchini China,
kutunga mipango ya maendeleo
ya uchumi na jamii ya taifa
wa kipindi cha miaka kadhaa
kumekuwa sera muhimu ya kusukuma
mbele maendeleo ya jamii ya
China, lakini mipango hiyo
inapaswa kuidhinishwa na bunge
la umma la China ndipo itakapoweza
kuonesha umuhimu wake wa kisheria.
Sheria ya China inaeleza kuwa,
viongozi wakuu wa China kama
vile rais wa nchi, spika wa
bunge la umma na wengineo
wanapaswa kuchaguliwa na bunge
la umma la China. Waziri mkuu
wa serikali na mawaziri mbalimbali
pia wanapaswa kuteuliwa na
Bunge la umma la taifa. Bunge
la umma la China pia linaweza
kupitisha utaratibu kutoa
mapendekezo ya kuwaondoa madarakani
spika wa bunge la umma, rais
wa nchi au waziri mkuu waliochaguliwa
au kuthibitishwa nalo.
Utaratibu wa ushirikiano
wa vyama vingi na mashauriano
ya kisiasa
Utaratibu wa ushirikiano
wa vyama vingi na mashauriano
ya kisiasa chini ya uongozi
wa Chama cha kikomunisti cha
China ni utaratibu wa kisiasa
wa kimsingi wa China.
China ni nchi yenye vyama
vingi. Mbali na Chama cha
kikomunisti cha China kinachotawala,
pia kuna vyama vinane vya
kidemokrasia. Vyama hivyo
vya kidemokrasia vilikuwepo
kabla ya kuzaliwa kwa Jamhuri
ya Watu wa China. Kisiasa,
vyama hivyo vinaunga mkono
uongozi wa chama cha kikomunisti,
hili ni chaguo lao la kihistoria
katika mchakato wa kufanya
ushirikiano wa muda mrefu
na juhudi za pamoja na chama
cha kikomunisti. Chama cha
kikomunisti cha China na vyama
mbalimbali vya kidemokrasia
vinapaswa kufuata kanuni za
katiba katika shughuli zao
za kimsingi. Vyama mbalimbali
vya kidemokrasia vyote vinajitawala
katika jumuiya zao, ambavyo
vina uhuru wa kisiasa, kijumuiya
na hadhi sawa ya kisheria
kutokana na katiba ya nchi.
Sera ya kimsingi ya ushirikiano
kati ya Chama cha kikomunisti
cha China na vyama mbalimbali
vya kidemokrasia ni “Kuwepo
pamoja kwa muda mrefu, kusimamiana,
kutendeana kwa udhati, kufaidika
na mafanikio na kukabiliana
na taabu kwa pamoja”.
Vyama mbalimbali vya kidemokrasia
vya China sivyo vyama visivyotawala
wala vyama vya upinzani, bali
ni vyama vinavyoshiriki mambo
ya siasa. Vyama hivyo vinaweza
kushiriki mashauirano kuhusu
utoaji wa sera kuu za taifa
na uchaguzi wa viongozi wa
nchi, kushiriki usimamizi
wa mambo ya taifa na kushiriki
katika utekelezaji wa siasa,
sera, sheria na kanuni za
taifa.
Wakati serikali kuu inapochukua
hatua kubwa au kuamua masuala
muhimu kuhusu mambo ya nchi
au maisha ya wananchi, Chama
cha kikomunisti cha China
hufanya mashauriano, kusikiliza
maoni na mapendekezo na vyama
vya kidemokrasia au watu wa
kidemokrasia wasio na vyama,
baadaye kutoa sera; wajumbe
wa vyama vya kidemokrasia
na watu wasio na vyama wanaweza
kuchaguliwa kuwa wajumbe katika
Bunge la umma la China, na
kamati mbalimbali za kudumu,
ili kushiriki vizuri zaidi
katika mambo ya siasa na kufanya
kazi ya usimamizi; vinaweza
kufanya kazi muhimu katika
Baraza la mashauriano ya kisiasa
na kushika nyadhifa mbalimbali
katika serikali za ngazi mbalimbali
na idara za utekelezaji wa
sheria.
Njia muhimu za ushirikiano
wa vyama vingi na mashauriano
ya kisiasa ni kama zifuatazo:
Kwanza, Baraza la mashauriano
ya kisiasa la umma. Baraza
hilo ni baraza muhimu la kushiriki
mambo ya siasa na utoaji wa
sera za taifa kwa vyama mbalimbali,
makundi mbalimbali ya umma
na wajumbe wa sekta mbaimbali;
Pili, makongamano na mikutano
inayoendeshwa na Kamati kuu
ya chama cha kikomunisti cha
China na kamati za chama za
ngazi mbalimbali. Kwenye makongamano
na mikutano hiyo, Chama cha
kikomunisti cha China husikiliza
maoni na mapendekezo ya vyama
mbalimbali na watu wasio na
vyama kuhusu hali muhimu nchini,
sera muhimu ya taifa, orodha
ya wateule wa viongozi wa
taifa na serikali za mitaa,
orodha ya wateule wa wajumbe
wa Bunge la umma na Baraza
la mashauriano ya kisiasa;
Tatu, wajumbe wa vyama mbalimbali
vya kidemokrasia kwenye Bunge
la umma la taifa wanaweza
kushiriki kwenye mambo ya
siasa na kufanya kazi ya usimamizi
katika bunge la umma la China
kwenye ngazi mbalimbali; Nne,
kuwateua wajumbe wa vyama
vya kidemokrasia kushika nyadhifa
katika Baraza la serikali
na wizara mbalimbali au serikali
za mitaa na idara husika;
Tano, kuwateua wajumbe wa
vyama vya kidemrokasia kushika
nyadhifa katika idara za uendeshaji
wa mashitaka na mahakama mbalimbali.
|