中国国际广播电台
Utaratibu wa Bunge la umma
la China ni utaratibu wa kisiasa
wa kimsingi wa China. Bunge
la umma la China ni chombo
chenye madaraka ya juu kabisa
la taifa, ambalo linaundwa
na wajumbe waliochaguliwa
kutoka mikoa, mikoa inayojiendesha,
miji inayotawaliwa moja kwa
moja na serikali kuu, mikoa
ya utawala maalum na jeshi.
Chombo hicho kinaendesha madaraka
ya taifa ya utungaji wa sheria
na kuamua masuala makubwa
ya maisha ya siasa ya taifa.
Madaraka makuu ya Bunge la
umma la China ni: Kurekebisha
katiba, kusimamia utekelezaji
wa katiba, kutunga na kurekebisha
sheria za makosa ya jinai,
mambo ya raia, idara za taifa
na sheria nyingine za kimsingi;
kuthibitisha na kuidhinisha
mipango ya maendeleo ya uchumi
na jamii na ripoti kuhusu
hali ya utekelezaji wa mipango,
pamoja na bajeti ya taifa
na ripoti kuhusu hali ya utekelezaji
wa bajeti ya taifa; kuidhinisha
kuanzishwa na kuwekwa kwa
mikoa, mikoa inayojiendesha
na miji inayotawaliwa moja
kwa moja na serikali kuu,
na kuamua uanzishaji wa mkoa
wa utawala maalum na mfumo
wake; kuamua masuala kuhusu
vita na amani; kuchagua na
kuamua viongozi wa chombo
chenye madaraka ya juu kabisa
cha taifa, yaani kuchagua
wajumbe wa Halmashauri ya
kudumu ya Bunge la umma la
China na wajumbe wa bunge
hilo, kuwachagua rais, makamu
wa rais wa nchi, kuamua waziri
mkuu wa serikali na viongozi
wengine, kuchagua mwenyekiti
wa kamati kuu ya kijeshi na
viongozi wengine wa kamati
hiyo, kumchagua mkuu wa mahakama
kuu ya umma na kumchagua mkuu
wa Idara kuu ya uendeshaji
wa mashitaka. Bunge la umma
la China lina madaraka ya
kuwaondoa madarakani viongozi
wote hao waliotajwa.
Muda wa Bunge la umma la
China la kila awamu ni miaka
mitano, bunge hilo linafanya
mkutano wa wajumbe wote kila
mwaka. Wakati mkutano huo
unapofungwa, Halamshauri yake
ya kudumu inaendesha madaraja
ya juu kabisa ya taifa. Halamshauri
ya kudumu ya Bunge la umma
la China linaundwa na spika,
manaibu maspika, katibu mkuu
na wajumbe.
Utungaji sheria wa China ni
pamoja na utungaji sheria
wa Bunge la umma la China
na halmashauri yake ya kudumu,
utungaji sheria wa Baraza
la serikali na wizara zake,
utungaji sheria wa kawaida
wa mikoa mbalimbali, utungaji
sheria wa mikoa inayojiendesha
ya makabila madogomadogo,
utungaji sheria wa sehemu
maalum za kiuchumi na mikoa
ya utawala maalum.
|