Baraza la mashaurinao ya kisiasa la umma la China

中国国际广播电台


Baraza la mashauriano ya kisiasa la umma la China ni jumuia ya wazalendo wanaopenda nchi ambalo ni baraza muhimu la kufanya ushirikiano wa vyama vingi na mashauriano ya kisiasa chini ya uongozi wa Chama cha kikomunisti cha China, ambapo wajumbe wa jumuia hiyo wanaweza kuenzi demokrasia ya ujamaa katika maisha ya siasa ya China. Mshikamano na demokrasia ni mada kubwa mbili za baraza hilo.


Halmashauri ya nchi zima ya Baraza la mashauriano ya kisiasa la umma la China inaundwa na wajumbe wa Chama cha kikomunisti cha China, vyama mbalimbali vya kidemokrasia, watu wasio na vyama, makundi ya umma, wajumbe wa makabila madogomadogo na wajumbe wa sekta mbalimbali, ndugu wa mikoa ya utawala maalum ya Hong Kong na Makau, ndugu wa Taiwan na wachina walioishi nchi za nje pamoja na watu walioalikwa maalum. Muda wa kila awamu ya halmashauri hiyo ni miaka mitano.

Jukumu kubwa la halmashauri hiyo na ya ngazi mbalimbali ni kufanya mashauriano ya kisiasa, usimamizi wa demokrasia, kutoa maoni na mapendekezo kuhusu sera za nchi na maazimio ya serikali.
Mashariano ya kisiasa
Kabla ya serikali kuu na serikali za mikoa kutoa sera na maazimio kuhusu masuala makubwa ya siasa, uchumi, utamaduni na jamii, Halmashauri ya nchi nzima ya Baraza la mashauriano ya kisiasa na halmashauri ya mikoa zinaweza kuitisha mikutano inayohudhuriwa na wakuu wa vyama mbalimbali na makundi mbalimbali pamoja na wajumbe wa makabila na sekta malimbali ili kufanya mashauriano na kutoa maoni na mapendekezo yao.

Usimamizi wa kidemokrasia:
Kutoa maoni na mapendekezo au ukosoaji kwa kufanya usimamizi kuhusu utekelezaji wa katiba ya nchi, sheria na kanuni, sera na hatua kubwa, kazi za ofisi za serikali na watumishi wake.

Kushiriki mambo ya siasa
Kufanya uchunguzi na utafiti na kufanya majadiliano kwa kutoa maoni ya wananchi kuhusu masuala muhimu ya siasa, uchumi, utamaduni na maisha ya jamii pamoja na masuala yanayofuatiliwa na umati wa watu. Kutoa ripoti na miswada ya mapendekezo au kupitia njia nyingi kwa kutoa maoni na mapendekezo kwa chama cha kikomunisti cha China na idara za serikali ya China.

Mwezi Septemba mwaka 1949, Mkutano wa kwanza wa wajumbe wote wa Baraza la mashauriano ya kiasiasa la umma la China uliendesha madaraka badala ya Bunge la umma la China na kuwakilisha nia ya wananchi wa taifa zima, ukitangaza kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China, hii ni kazi muhimu ya historia iliyofanywa na baraza hilo. Baada ya kufanyika kwa mkutano wa kwanza wa Bunge la umma la China mwaka 1954, Baraza la mashauriano ya kisiasa haliendeshi tena madaraka ya Bunge la umma la China, lakini limeendelea kuwepo likiwa jumuiya ya wazalendo wanaoipenda nchi, ambalo limefanya kazi nyingi na kutoa mchango mkubwa katika maisha ya kisiasa ya taifa na maisha ya jamii pamoja na shughuli za urafiki kwa nchi za nje. Ilipofika mwezi Machi mwaka 2004, baraza hilo limeanzisha mawasiliano na idara 170 za nchi 101 na jumuia 8 za kimataifa au kikanda, na kuanzisha mawasiliano ya kirafiki.