中国国际广播电台
Baraza la serikali
Baraza la serikali la China
yaani serikali kuu ya umma,
ni chombo kikuu cha mambo
ya utawala cha nchi. Baraza
hilo linatekeleza sheria na
maazimio yaliyopitishwa na
Bunge la umma la China na
halmashauri yake ya kudumu,
na kuwajibika pia kutoa ripoti
ya kazi kwa Bunge la umma
la China na halmashauriano
yake ya kudumu,. Baraza la
serikali lina madaraka ya
kuweka hatua za utawala, kubuni
sheria na kanuni za utawala,
na kutoa maazimio na maagizo
ndani ya madaraka yake. Baraza
la serikali linaundwa na waziri
mkuu, manaibu mawaziri, wajumbe
wa kitaifa, mawaziri wa wizara
mbalimbali, wakurugenzi wa
kamati mbalimbali, mkaguzi
mkuu wa uhasibu, na katibu
mkuu. Waziri mkuu wa hivi
sasa ni Bwana Wen Jiabao.
Hivi sasa Baraza la serikali
la China linaundwa na wizara
na kamati 28 kama vile Wizara
ya mambo ya nje, Wizara ya
ulinzi wa taifa, Kamati ya
maendeleo na mageuzi ya taifa,
Wizara ya elimu, Wizara ya
sayansi na teknolojia, Kamati
ya viwanda vya sayansi na
teknolojia za ulinzi wa taifa,
Kamati ya mambo ya makabila
madogomadogo, Wizara ya usalama
wa umma, Wizara ya usalama
wa nchi, Wizara ya mambo ya
kiraia, Wizara ya sheria,
Wizara ya fedha, Wizara ya
ajira, Wizara ya kazi na huduma
za jamii, Wizara ya reli,
Wizara ya mawasiliano, Wizara
ya maliasili ya ardhi ya taifa,
Wizara ya ujenzi, Wizara ya
shughuli za upashanaji habari,
Wizara ya maji, Wizara ya
utamaduni, Wizara ya afya,
Wizara ya Kilimo, Wizara ya
biashara, Kamati ya idadi
ya watu na uzazi wa mpango,
Benki ya umma ya China na
Idara kuu ya ukaguzi wa uhasibu.
Wizara ya mambo ya
nje
Wizara ya mambo ya nje ni
wizara ya Baraza la serikali
inayowajibika na utekelezaji
wa sera za China kwa nchi
za nje na kushughulikia kazi
ya kiplomasia ya kila siku.
Jukumu kuu la wizara hiyo
ni kuwakilisha taifa na serikali
kusimamia mambo ya kidiplomasia
kama vile kutangaza sera na
maamuzi ya taifa kwa nchi
za nje, kutangaza nyaraka
na taarifa kuhusu mambo ya
kidiplomasia; kushughulikia
mambo ya kidiplomasia na kufanya
mawasiliano ya kidiplomasia,
kusaini mikataba, makubaliano
na nyaraka nyingine za kidiplomasia;
kuhudhuria mikutano ya kimataifa
ya Umoja wa Mataifa na kati
ya serikali na serikali na
kushiriki kwenye shughuli
za jumuiya za kimataifa; kushughulikia
kazi ya kuanzisha ubalozi
na ofisi husika za wawakilishi
katika nchi za nje, kuwasimamia
watumishi wa serikali wanaofanya
kazi katika idara hizo, kuelekeza,
kushirikisha na kuratibu shughuli
za kidiplomasia kati ya idara
za mambo ya nje katika wizara
mbalimbali za Baraza la serikali
na mikoa, mikoa inayojiendesha
na miji inayotawaliwa moja
kwa moja na serikali kuu,
na kushughulikia kazi ya kuwaandaa
na kuwasimamia makada wa kidiplomasia.
Waziri wa mambo ya nje wa
China wa hivi sasa ni Bwana
Li Zhaoxing.
Kamati ya maendeleo
na mageuzi ya nchi
Jukumu la kamati hiyo ni kubuni
na kutekeleza mikakati ya
maendeleo ya uchumi na jamii,
mipango ya muda mrefu na wastani
na mipango ya mwaka; kufanya
utafiti na uchambuzi kuhusu
hali ya uchumi wa nchini na
ng’ambo na maendeleo ya hali
hiyo, kufanya makadirio na
kutoa tahadhari kuhusu uchumi
wa taifa; kufanya utafiti
kuhusu masuala muhimu yanayohusika
na usalama wa uchumi wa taifa,
kutoa mapendekezo kuhusu sera
za marekebisho na udhibiti
wa uchumi, kufanya usawazishaji
wa maendeleo ya uchumi na
jamii; kufanya mipango kuhusu
miradi mikubwa na nguvu kazi
nchini; kufanya mipango kuhusu
fedha za ujenzi za taifa,
kuelekeza na kusimamia matumizi
ya fedha za mikopo kutoka
nchi za nje kwa ujenzi wa
China, na kuelekeza na kusimamia
mwelekeo wa matuizi ya mikopo
ya kisera; kuelekeza mwelekeo
wa fedha za raia katika uwekezaji
wa mali zisizohamishika; kufanya
utafiti na kutoa malengo na
sera za kimkakati kuhusu matumizi
ya mitaji na uwekezaji kutoka
nje; kupanga miradi ya ujenzi
inayogharimiwa na serikali
na miradi mikubwa ya ujenzi,
miradi mikubwa ya uwekezaji
wa nje, miradi ya uendelezaji
wa maliasili na miradi ya
uwekezaji mkubwa katika nchi
za nje; kubuni na kutunga
sheria na kanuni husika za
utawala kuhusu maendeleo ya
uchumi na jamii ya taifa pamoja
na mageuzi ya mfumo wa uchumi,
kuzifungulia mlango nchi za
nje, na kushiriki kazi za
kutunga sheria na kanuni za
utawala na utekelezaji.
Mkurugenzi wa sasa wa Kamati
ya maendeleo na mageuzi ya
taifa ni Bwana Ma Kai.
Wizara ya biashara
Wizara hiyo ilianzishwa rasmi
mwezi Machi mwaka 2003.
Jukumu lake kuu ni kubuni
mikakati, mwongozo na sera
kuhusu maendeleo ya biashara
nchini na ng’ambo na ushirikiano
wa kimataifa wa sekta ya uchumi,
kutunga sheria na kanuni kuhusu
biashara ya nchini na ng’ambo,
ushirikiano wa kiuchumi wa
kimataifa na uwekezaji wa
wafanyabiashara kutoka nje;
kubuni mipango ya maendeleo
ya biashara ya nchini, kufanya
utafiti na kutoa maoni kuhusu
mageuzi ya utaratibu wa mzunguko
wa bidhaa, kuandaa na kuendeleza
soko mijini na vijijini; kufanya
utafiti kwa kubuni sera kuhusu
utaratibu kamili wa uendeshaji
wa soko, utaratibu wa mzunguko
wa bidhaa na kuvunja ukiritimba
wa soko na vikwazo vya kisehemu,
kujenga mfumo wa soko wenye
utaratibu kamili, wa kufunguliwa
mlango na wa ushindani; kufuatilia
na kuchambua hali ya uendeshaji
wa soko na hali ya utoaji
wa bidhaa sokoni, kutekeleza
hatua za marekebisho na udhibiti
kuhusu bidhaa muhimu za matumizi
sokoni na usimamizi wa mzunguko
wa raslimali muhimu za uzalishaji;
kufanya utafiti na kubuni
njia za usimamizi wa bidhaa
ziagizwazo kutoka nje na ziuzwazo
kwa nje pamoja na orodha ya
bidhaa hizo, kutekeleza mipango
ya mgao wa kuagiza bidhaa
na kuuza bidhaa, kuthibitisha
kiasi cha mgao na kutoa kadi
za kibali; kutunga na kutekeleza
sera kuhusu zabuni ya mgao
wa bidhaa ziagizwazo kutoka
nje na ziuzwazo kwa nje; kuratibu
kazi ya kupinga mauzo ya bidhaa
nyingi za bei chini, kupinga
utoaji ruzuku, kutoa hatua
za uhakikishaji na kazi nyingine
zinazohusika na biashara ya
haki, kuanzisha utaratibu
wa utoaji tahadhari kuhusu
biashara ya haki, kufanya
uchunguzi kuhusu hasara za
mashirika; kuelekeza na kuratibu
kazi ya kujibu mashitaka kuhusu
bidhaa za China zilizouzwa
nje na kazi nyingine zinazohusika.
|