Kamati ya kijeshi ya kamati kuu ya chama

中国国际广播电台


Kamati ya kijeshi ya kamati kuu ya Chama cha kikomunsti cha China ni idara kuu ya uongozi wa kijeshi chini ya uongozi wa Chama cha kikomunisti cha China, kamati hiyo inaundwa na mwenyekiti, naibu mwenyekiti na wajumbe. Kamati hiyo inaamuliwa na kamati kuu ya Chama cha kikomunisti cha China, ambayo inatekeleza utaratibu wa mwenyekiti kubeba wajibu. Jukumu lake kuu ni kuongoza moja kwa moja nguvu za majeshi ya nchi nzima.

Kamati kuu ya kijeshi ya Jamhuri ya Watu wa China ni idara ya uongozi wa kijeshi wa taifa, ambayo inaongoza nguvu za majeshi ya nchi nzima. Kamati hiyo inaundwa na mwenyekiti, manaibu wenyekiti kadhaa, na wajumbe kadhaa. Kamati hiyo inatekeleza utaratibu wa mwenyekiti kubeba wajibu. Mwenyekiti wa kamati hiyo huchaguliwa kwenye mkutano wa Bunge la umma la China, ambaye anawajibika kwa Bunge la umma la China na halmashauri yake ya kudumu. Muda wa kamati kuu ya kijeshi ya kila awamu ni miaka mitano, lakini hakuna kikomo kuhusu kiasi cha awamu.

Nguvu za majeshi ya China zinaundwa na Jeshi la ukombozi wa umma la China, Kikosi cha askari polisi cha umma cha China na wanamgambo. Jeshi la ukombozi wa umma ni jeshi la kudumu la taifa; kikosi cha askari polisi kinabeba jukumu la taifa la kulinda usalama na utaratibu wa jamii; wanamgambo ni wa kundi la umati wa watu wasiojitenga na shughuli za uzalishaji mali.
Mwenyekiti wa sasa wa Kamati ya kijeshi ya Kamati kuu ya Chama cha kikomunisti cha China na Kamati kuu ya kijeshi ya Jamhuri ya watu wa China ni Bwana Xi Jinping.