中国国际广播电台
Kamati ya kijeshi ya kamati
kuu ya Chama cha kikomunsti
cha China ni idara kuu ya
uongozi wa kijeshi chini ya
uongozi wa Chama cha kikomunisti
cha China, kamati hiyo inaundwa
na mwenyekiti, naibu mwenyekiti
na wajumbe. Kamati hiyo inaamuliwa
na kamati kuu ya Chama cha
kikomunisti cha China, ambayo
inatekeleza utaratibu wa mwenyekiti
kubeba wajibu. Jukumu lake
kuu ni kuongoza moja kwa moja
nguvu za majeshi ya nchi nzima.
Kamati kuu ya kijeshi ya
Jamhuri ya Watu wa China ni
idara ya uongozi wa kijeshi
wa taifa, ambayo inaongoza
nguvu za majeshi ya nchi nzima.
Kamati hiyo inaundwa na mwenyekiti,
manaibu wenyekiti kadhaa,
na wajumbe kadhaa. Kamati
hiyo inatekeleza utaratibu
wa mwenyekiti kubeba wajibu.
Mwenyekiti wa kamati hiyo
huchaguliwa kwenye mkutano
wa Bunge la umma la China,
ambaye anawajibika kwa Bunge
la umma la China na halmashauri
yake ya kudumu. Muda wa kamati
kuu ya kijeshi ya kila awamu
ni miaka mitano, lakini hakuna
kikomo kuhusu kiasi cha awamu.
Nguvu za majeshi ya China
zinaundwa na Jeshi la ukombozi
wa umma la China, Kikosi cha
askari polisi cha umma cha
China na wanamgambo. Jeshi
la ukombozi wa umma ni jeshi
la kudumu la taifa; kikosi
cha askari polisi kinabeba
jukumu la taifa la kulinda
usalama na utaratibu wa jamii;
wanamgambo ni wa kundi la
umati wa watu wasiojitenga
na shughuli za uzalishaji
mali.
Mwenyekiti wa sasa wa Kamati
ya kijeshi ya Kamati kuu ya
Chama cha kikomunisti cha
China na Kamati kuu ya kijeshi
ya Jamhuri ya watu wa China
ni Bwana Xi Jinping.
|