Mahakama kuu ya umma

中国国际广播电台



Mahakama kuu ya umma ni idara ya taifa ya kushughulikia kesi. Serikali inaweka mahakama kuu ya umma, mikoa, mikoa inayojiendesha na miji inayotawaliwa moja kwa moja na serikali kuu inaweka mahakama kuu ya ngazi ya juu, mahakama ya umma ya ngazi ya kati na mahakama ya umma ya shina. Mahakama kuu ya umma ni chombo cha taifa cha hukumu cha ngazi ya juu kabisa, ambayo inaendesha madaraka ya uhukumu bila kuingiliwa, vilevile ni mamlaka ya juu kabisa ya usimamizi wa kazi ya mahakama ya umma ya ngazi mbalimbali. Mahakama kuu ya umma inawajibika kwa Bunge la umma la China na kutoa ripoti kuhusu kazi yake kwa bunge la umma, mkuu na naibu mkuu wa Mahakama kuu ya umma pamoja na wajumbe wa Kamati ya utoaji hukuma wa Mahakama kuu ya umma wote wanateuliwa na kuamuliwa na Bunge la umma la umma la China.
Jukumu la Mahakama kuu ya umma ni kushughulikia kazi ya utoaji hukumu kuhusu kesi zilizotolewa rufaa juu ya hukumu zilizotolewa na mahakama za ngazi ya Chini au Idara kuu ya uendeshaji wa mashitaka ya umma kwa kufuata utaratibu wa usimamizi wa hukumu; kuthibitisha hukumu za vifo; kama kugundua makosa katika hukumu zilizotolewa na mahakama ya umma ya ngazi mbalimbali, mahakama kuu ya umma ina madaraka ya kuhukumu au kuagiza mahakama ya ngazi ya chini kuhukumu tena; kuthibitisha uhalifu; na kutoa ufafanuzi kuhusu namna ya kutumia sheria halisi katika mchakato wa hukumu na kadhalika.
Mkuu wa Mahakama kuu ya umma wa sasa ni Bwana Xiao Yang.