Idara ya uendeshaji wa mashitaka ya umma

中国国际广播电台



Idara ya uendeshaji wa mashitaka ya umma ni mamlaka ya taifa ya usimamizi wa sheria. Idara hiyo inakamilisha jukumu lake kwa kuendesha madaraka yake ya uendeshaji wa mashitaka. Idara hiyo inaendesha madaraka yake katika kesi ya kuhaini nchi, kufarakanisha taifa na kesi nyingine kubwa; kufanya ukaguzi na uthibitishaji kuhusu kesi zilizoshughulikiwa na idara za usalama wa umma, kuamua kuwakamata watuhumiwa, kuwashitaki au kutowashitaki; kufanya usimamizi kuhusu shughuli za idara za usalama wa umma, mahakama ya umma, magereza na idara husika za utekelezaji wa sheria.
Idara kuu ya uendeshaji wa mashitaka inaendesha madaraka yake bila kuingiliwa kwa mujibu wa sheria, kazi yake hairuhusiwi kuingiliwa na idara za utawala, makundi ya jamii au watu binafsi; na inatekeleza sheria kwa raia wote kwa usawa. Serikali kuu inagawanyika katika Idara kuu ya uendeshaji wa mashitaka ya umma, idara za uendeshaji wa mashitaka za mitaa za ngazi mbalimbali na idara ya kijeshi ya uendeshaji wa mashitaka. Idara za uendeshaji wa mashitaka za umma za China zinagawanyika katika ngazi nne, yaani idara za shina, idara ya ngazi ya kati, idara ya ngazi ya juu na idara kuu ya uendeshaji mashitaka. Idara kuu ya uendeshaji wa mashitaka ni idara ya juu kabisa ya taifa yenye madaraka ya kuendesha mashitaka, ikiwakilisha taifa kuendesha madaraka ya uendeshaji wa mashitaka kwa kujiamulia, inawajibika moja kwa moja kwa Halmashauri ya kudumu ya Bunge la umma la China. Jukumu lake kuu ni kuongeza idara za uendeshaji mashitaka za ngazi mbalimbali za mitaa na idara maalum za uendeshaji wa mashitaka kutekeleza wajibu wake wa usimamizi wa kisheria, na kuhakikisha kuwa sheria za pamoja za taifa na utekelezaji wake sahihi.
Mkuu wa sasa wa Idara kuu ya uendeshaji wa mashitaka ya umma ni Bwana Jia Chunwang.