中国国际广播电台
Chama cha kikomunisti cha China
ni chama cha watangulizi wa
tabaka la wafanyakazi wa China,
pia ni chama cha watangulizi
wa wananchi wa China na taifa
la China. Chama hicho ni kiini
cha uongozi wa jitihada za ujenzi
wa mambo ya ujamaa wenye umaalum
wa kichina, ambacho kinawakilisha
matakwa ya maendeleo ya nguvukazi
ya kisasa ya China, kuwakilisha
mwelekeo wa kusonga mbele wa
utamaduni wa kisasa wa China
na kuwakilisha maslahi ya kimsingi
ya wanachi wengi kabisa wa China.
Tumainio kubwa kabisa na
lengo la mwisho la Chama cha
kikomunisti cha China ni kutimiza
ukomunisti. Katiba ya chama
hicho inaeza kuwa, dira ya
vitendo vya Chama cha kikomunisti
cha China ni Umax-Lenin, Fikra
Mao Zedong, Nadharia ya Deng
Xiaoping na wazo muhimu la
“Uwakilishi mtatu”.
Chama cha kikomunsti cha
China kilizaliwa mwezi Julai
mwaka 1921. Toka mwaka 1921
hadi 1949, chama hiki kiliwaongoza
wananchi wa China katika kufanya
mapambano magumu, na kupindua
utawala wa ubeberu, umwinyi
na ubepari wa utawala msonge,
hatimaye kuanzisha Jamhuri
ya Watu wa China. Baada ya
kuzaliwa kwa Jamhuri ya Watu
wa China, Chama cha kikomunsti
cha China kiliwaongoza wananchi
wa makabila mbalimbali wa
nchi nzima katika kulinda
uhuru na usalama wa nchi,
kufanikiwa kuiwezesha jamii
ya China ibadilike kuwa jamii
ya ujamaa badala ya jamii
ya demokrasia mpya, na kuanzisha
ujenzi mkubwa wa ujamaa kwa
kufuata mipango, na kuyafanya
mambo ya uchumi na utamaduni
ya China yapate maendeleo
makubwa sana ambayo hayakupatikana
katika historia.
Baada ya kukamilisha kimsingi
mageuzi ya kiujamaa ya mfumo
wa umilikaji wa binafsi wa
raslimali za uzalishaji mwaka
1956, kutokana na ukosefu
wa uzoefu, Chama cha kikomunisti
cha China kiliwahi kufanya
makosa kadhaa katika mchakato
wa kuongoza ujenzi wa ujamaa;
na makosa makubwa yaliyowahi
kufanyika ni “mapinduzi makubwa
ya utamaduni” kote nchini
kwa muda mrefu, tokea mwaka
1966 hadi 1976.
Mwezi Oktoba mwaka 1976, “mapinduzi
makubwa ya utamaduni” yalikomeshwa,
China ikaingia katika kipindi
kipya cha maendeleo ya historia.
Baada ya kufanyika kwa mkutano
wa 3 wa wajumbe wote wa Kamati
kuu ya 11 ya Chama cha kikomunisti
cha China mwishoni mwa mwaka
1978, mabadiliko makubwa yenye
umuhimu mkubwa yalipatikana
tangu kuanzishwa kwa Jamhuri
ya Watu wa China. Kuanzia
mwaka 1979, Chama cha kikomunisti
cha China kilitekeleza sera
iliyopendekezwa na Deng Xiaoping
kuhusu kufanya mageuzi na
kuzifungulia mlango nchi za
nje. Tokea sera hiyo ianze
kutekelezwa, mafanikio makubwa
ya kuvutia dunia nzima yalipatikana
katika maendeleo ya uchumi
na jamii ya China, ambapo
sura ya nchi ilipata mabadiliko
makubwa kabisa, kipindi hiki
ni kipindi chenye hali nzuri
kabisa tangu kuzaliwa kwa
Jamhuri ya Watu wa China,
vilevile ni kipindi ambacho
wananchi walipata manufaa
makubwa kabisa.
Chama cha kikomunisti cha
China kinatetea kufanya juhudi
za kuendeleza uhusiano na
nchi za nje na kufanya juhudi
za kujipatia mazingira ya
kimataifa yanayosaidia mageuzi
na ufunguaji mlango na ujenzi
wa mambo ya kisasa ya China.
Katika mambo ya kimataifa,
Chama cha kikomunisti cha
China kinashikilia sera ya
kidiplomasia ya amani ya kujitawala
na kujiamulia mambo, kulinda
uhuru na mamlaka ya nchi ya
China, kupinga umwamba na
siasa ya mabavu, kulinda amani
ya dunia na kusukuma mbele
maendeleo ya binadamu; kuendeleza
uhusiano na nchi mbalimbali
duniani kwa msingi wa kanuni
tano za kuheshimu mamlaka
ya nchi na ukamilifu wa ardhi,
kutoshambuliana, kutoingiliana
mambo ya ndani, kuwa na usawa
na kunufaishana, na kuishi
pamoja kwa amani. Chama cha
kikomunisti cha China kimeanzisha
na kuendeleza uhusiano wa
kirafiki na vyama vya nchi
mbalimbali kwa kufuata kanuni
nne za kujitawala na kujiamulia,
kuwa na usawa kabisa, kuheshimiana
na kutoingiliana mambo ya
ndani. Hivi sasa Chama cha
kikomunisti cha China kimedumisha
mawasiliano ya kirafiki na
vyama zaidi ya 300 vya nchi
zaidi ya 120 duniani.
Chama cha kikomunisti cha
China ni umoja unaojumuika
kwa kufuata mwongozo na katiba
yake na utaratibu wa utawala
wa kidemokasia. “Katiba ya
Chama cha kikomunisti cha
China” inaeleza kuwa, watangulizi
wa wafanyakazi, wakulima wanajeshi,
wasomi na wengine wa jamii,
yeyote aliyetimia umri wa
miaka 18, anayetambua mwongozo
na katiba ya chama, anayependa
kujiunga na jumuiya ya chama
na kufanya kazi kwa bidii
ndani yake, anayetekeleza
maazimio ya chama na kutoa
ada ya mwanachama kwa wakati,
anaweza kutoa ombi la kujiunga
na Chama cha kikomunisti cha
China.
Vyombo vya kamati kuu ya chama
ni pamoja na Bunge la umma
la China, Kamati kuu ya chama,
Ofisi ya siasa ya Kamati kuu
ya chama, Kamati ya kudumu
ya Ofisi ya siasa ya kamati
kuu ya chama, Sekretarieti
ya Kamati kuu ya chama, Kamati
ya kijeshi ya Kamati kuu ya
chama na Kamati kuu ya ukaguzi
wa nidhamu. Mkutano wa wajumbe
wa nchi nzima wa chama unafanyika
mara moja kila mwaka. Wakati
mkutano huo unapofungwa, Kamati
kuu ya chama ni chombo cha
uongozi wa juu kabisa cha
Chama cha kikomunisti cha
China.
Chama cha kikomunisti cha
China hivi sasa kina wanachama
karibu milioni 70, katibu
mkuu wa chama hicho ni Xi Jinping.
|