中国国际广播电台
Nchini China mbali na Chama
cha kikomunnisti cha China,
pia kuna vyama vinane vya
kisiasa yaani vyama vya kidemokrasia
kama vile Kamati ya mapinduzi
ya Chama cha Guomintang cha
China, Umoja wa demokrasia
wa China, Shirikisho la kujenga
nchi ya kidemokrasia la China,
Shirikisho la kuhimiza demokrasia
la China, Chama cha demokrasia
cha wakulima na wafanyakazi
cha China, Chama cha Zhigong
cha China, Shirikisho la elimu
la Jiusan na Umoja wa kujiendesha
kidemokrasia wa Taiwan. Vyama
hivyo vingi vilianzishwa na
kuendelea wakati wa mapambano
dhidi ya uvamizi wa Japan
na katika vita vya ukombozi
wa nchi nzima. Vyama vya kidemokrasia
vinaunga mkono uongozi wa
Chama cha kikomunisti cha
China, hili ni chaguo lao
cha kihistoria katika ushirikiano
wa muda mrefu na juhudi za
pamoja. Vyama mbalimbali vya
kidemokrasia vinafaidika na
uhuru wa kisiasa, uhuru wa
kujitawala kijumuia na usawa
wa hadhi ya kisheria katika
eneo lililowekwa kwenye katiba
ya nchi. Chama cha kikomunisti
cha China na vyama mbalimbali
vya kidemokrasia vinafuata
sera ya kimsingi
ya ushirikiano ya “kuwepo
kwa pamoja kwa muda mrefu,
kusimamiana, kutendeana kwa
moyo safi na udhati, na kushirikiana
kwenye dhiki na faraja”.
Vyama mbalimbali vya kidemokrasia
si vyama visivyo vya tawala,
wala vyama vya upinzani, isipokuwa
ni vyama vinavyoshiriki mambo
ya kisiasa na utoaji wa sera.
Hivi sasa wanachama wengi
wa vyama mbalimbali vya kidemokrasia
wanashika nyadhifa mbalimbali
katika Bunge la umma la China
na Baraza la mashauriano ya
kisiasa kwenye ngazi mbalimbali,
vyombo vya serikali na idara
za uchumi, utamaduni, elimu,
sayansi na teknolojia, kwa
mfano wenyekiti wa kamati
kuu ya vyama vinane vya kidemokrasia
hivi sasa wanashika nyadhifa
za manaibu spika wa Bunge
la umma la China au manaibu
wenyeviti wa Baraza la mashauriano
ya kisiasa la China. Wakati
huo huo, matawi ya vyama mbalimbali
vya kidemokrasia pia yanaendelea
vizuri katika mikoa na miji
mbalimbali nchini China.
Kamati ya Mapinduzi
ya Chama cha Guomintang cha
China
Kamati ya Mapinduzi ya Chama
cha Guomintang cha China kwa
ufupi inaitwa Minge, ambacho
kilianzishwa tarehe 1 Januari,
mwaka 1948, kilianzishwa na
kundi la kidemokrasia la Chama
cha Guomintang cha China na
wazalendo wengine, chama hicho
kina umaalum wa shirikisho
la kisiasa, ambacho ni chama
kinachofanya juhudi katika
kujenga ujamaa na kutimiza
muungano wa taifa. Chama hicho
kina wanachama karibu elfu
65. Mwenyekiti wa kamati kuu
ya chama hicho ni Bibi He
Luli.
Umoja wa demokrasia
wa China
Umoja wa demokrasia wa China
kwa ufupi unaitwa Minmeng,
ambao ulianzishwa mwezi Machi,
mwaka 1941, wakati huo umoja
huo uliitwa “Shirikisho la
vikundi vya kisiasa vya kidemokrasia
la China”, mwaka 1944 uliundwa
upya na kubadilisha jina kuwa
Umoja wa demokrasia wa China.
Umoja huo ni umoja wa kisiasa
wa wasomi wanaoshughulikia
mambo ya utamaduni na elimu
na wazalendo wanaounga mkono
ujamaa, na ni chama chenye
malengo ya kijamaa. Idadi
ya wanachama wake ni laki
1.56. Mwenyekiti wake ni Bwana
Ding Shisun.
Shirikisho la kujenga
nchi ya kidemokrasia la China
Kwa ufupi shirikisho hilo
linaitwa Minjian, ambalo lilianzishwa
mwezi Desemba mwaka 1945,
wanachama wake wengi ni wanakampuni
na wafanyabiashara wazalendo
na wasomi wanaowasiliana nao.
Wanachama wake wamefikia elfu
85. Mwenyekiti wake wa hivi
sasa ni Bwana Cheng Siwei.
Shirikisho la uhimizaji
wa demokrasia la China
Shirikisho hilo linaitwa Minjin
kwa ufupi, ambalo lilianzishwa
mwezi Desemba mwaka 1945,
wanachama wake wengi ni wasomi
wa kiwango cha juu na wastani
wanaoshughulikia mambo ya
elimu, utamaduni, uchapishaji
vitabu na sayansi. Shirikisho
hilo lina wanachama elfu 81.
Mwenyekiti wake wa hivi sasa
ni Bwana Xu Jialu.
Chama cha demokrasia
cha wakulima na wafanyakazi
cha China
Chama hicho kinaitwa chama
cha Nonggong, ambacho kilianzishwa
mwezi Agosti mwaka 1930. Chama
hicho ni shirikisho la kisiasa
la wasomi wa kiwango cha juu
na wastani wanaoshughulikia
mambo ya afya, sayansi na
teknolojia na utamaduni na
elimu pamoja na wazalengo
wanaounga mkono ujamaa. Idadi
ya wanachama wake ni zaidi
ya elfu 80. Mwenyekiti wake
wa hivi sasa ni Bwana Jiang
Zhenghua.
Chama cha Zhigong
cha China
Chama hicho kilianzishwa mwezi
Oktoba mwaka 1925, ambacho
kiliundwa na wachina waliowahi
kuishi ng’ambo na jamaa zao.
Idadi ya wanachama wake ni
zaidi ya elfu 20. Mwenyekiti
wake wa hivi sasa ni Bwana
Luo Haocai.
Shirikisho la elimu
la Jiusan
Chama hicho kilianzishwa mwezi
Machi mwaka 1946, wanachama
wake ni zaidi ya elfu 80 ambao
ni wasomi wa kiwango cha juu
na wastani wanaoshughulikia
mambo ya sayansi na teknolojia,
utamaduni na elimu pamoja
na afya. Mwenyekiti wake wa
hivi sasa ni Bwana Han Qide.
Umoja wa kujiendesha
kidemokrasia wa Taiwan
Umoja huo unaitwa Taimeng
kwa ufupi, ambao ulianzishwa
mwezi Novemba mwaka 1947.
Umoja huo ni shirikisho la
kisiasa linaloundwa na wazalendo
wanaounga mkono ujamaa wa
mkoa wa Taiwan wanaoishi China
bara. Mwenyekiti wake wa sasa
ni Bwana Zhang Kehui.
Vikundi vya Jamii
Shirikisho kuu la
wafanyakazi wa China
Shirikisho kuu la wafanyakazi
wa China linaitwa Qiuanzong
kwa ufupi, ambalo ni chombo
cha uongozi cha mashirikisho
ya wafanyakazi ya sehemu mbalimbali
nchini China, ambalo lilianzishwa
tarehe 1 Mei, mwaka 1925.
Jukumu la shirikisho hilo
la jamii ni kulinda haki na
maslahi halali ya wafanyakazi
na haki zao za kidemokrasia;
kuwahamasisha na kuwashirikisha
wafanyakazi kushiriki katika
ujenzi na mageuzi, kukamilisha
majukumu ya maendeleo ya uchumi
na jamii; kushiriki kwenye
usimamizi wa kidemokrasia
ya mashirika, na kuwaelimisha
wafanyakazi wainue kiwango
cha maadili na elimu ya sayansi,
tekenolojia na utamaduni.
Shirikisho kuu la wafanyakazi
wa taifa la China limeanzisha
mawasiliano na uhusiano wa
kirafiki na mashirikisho ya
wafanyakazi ya kitaifa ya
nchi na sehemu zaidi ya 130
duniani. Ilipofika mwishoni
mwa mwaka 2002, idadi ya jumla
ya wanachama wa shirikisho
hilo imefikia milioni 134.
Mwenyekiti wa hivi sasa wa
shirikisho hilo ni Bwana Wang
Zhaoguo.
Shirikisho kuu la
vijana la taifa la China
Shirikisho hilo lilianzishwa
tarehe 4 Mei mwaka 1949 ambalo
ni shirikisho la vijana wa
makabila mbalimbali wa China.
Jukumu kuu la shirikisho hilo
ni kuwakilisha na kulinda
haki na maslahi ya vijana
wa makabila mbalimbali na
sekta mbaimbali za China;
kuwaelekeza vijana wafanye
juhudi na kushiriki kwenye
maisha ya jamii, kufanya juhudi
za kuwahudumia vijana kwa
ajili ya ukuaji wao mzuri
na kuwa watu wenye ujuzi kwa
kulitumikia taifa; kuimarisha
mawasilliano na mshikamano
na vijana wa Taiwan, Hong
Kong na Makau pamoja vijana
wanaoishi ng’ambo; na kuendeleza
mawasiliano na urafiki ma
vijana wa nchi mbalimbali
duniani.
Kamati ya nchi nzima ya shirikisho
kuu la vijana ni chombo chenye
madaraka ya juu kabisa, muda
wake wa kila awamu ni miaka
mitano. Kamati hiyo ina mwenyekiti
mmoja na manaibu wenyeviti
kadhaa. Wakati wa kufungwa
kwa kamati hiyo, halmashauri
ya kudumu ya kamati hiyo inaendesha
shughuli zake za kila siku.
Shirikisho hilo linatekeleza
utaratibu wa wanachama wa
makundi, hivi sasa kuna wanachama
wa makundi 48, wajumbe 1352,
mwenyekiti wake wa hivi sasa
ni Bwana Sun Jinlong.
Shirikisho kuu la
kina mama wa taifa zima la
China
Shirikisho hilo lilianzishwa
mwezi Machi mwaka 1949, jina
lake la mwanzoni ni Shirikisho
kuu la kina mama la kidemokasia
la taifa la China, mwaka 1957
jina lake lilibadilishwa kuwa
Shirikisho kuu la kina mama
la Jamhuri ya Watu wa China,
mwaka 1978 jina lake lilibadilishwa
kuwa Shirikisho kuu la kina
mama la taifa zima la China.
Jukumu lake la kimsingi ni:
Kuleta mshikamano, kuhamasisha
kina mama wengi washiriki
katika ujenzi wa uchumi na
maendeleo ya jamii, kuwakilisha
na kulinda haki na maslahi
ya kina mama, na kusukuma
mbele usawa kati ya wanaume
na wanawake.
Mwenyekiti wa sasa wa shirikisho
kuu hilo ni Bibi Gu Xiulian.
Shirikisho kuu la
viwanda na biashara la taifa
la China
Shirikisho hilo lilianzishwa
mwaka 1953, ambalo ni kundi
la umma na shirikisho la biashara
la kiraia lililoundwa na watu
wa sekta za viwanda na biashara
wa China.
Jukumu kuu la shirikisho hilo
ni kushiriki kwenye mashauriano
ya kisiasa, kutoa maoni na
mapendekezo na kufanya usimamizi
kuhusu sera na hatua kubwa
za nchi na masuala makubwa
kuhusu siasa, uchumi na maisha
ya jamii; kuwaelekeza wanachama
wake wafanye juhudi za kushiriki
katika ujenzi wa uchumi wa
nchi, kusukuma mbele kazi
ya kukamilisha siku hadi siku
mfumo wa uchumi wa soko huria
wa ujamaa, kusukuma mbele
maendeleo ya jamii kwenye
sekta zote; kuwakilisha haki
na maslahi halali ya wanachama
wake, kueleza maoni, matakwa
na mapendekezo ya wanachama
wake; kutoa huduma mbalimbali
kwa wanachama wake; kuanzisha
mafunzo ya kazi maalum, kuwasaidia
wanachama wake kuboresha usimamizi
na uendeshaji wa shughuli,
kukamilisha usimamizi wa kazi
ya uhasibu, na kuinua teknolojia
za uzalishaji na sifa za bidhaa;
kuongeza mawasiliano na urafiki
na mashirika ya viwanda na
biashara na mikoa ya utawala
maalum ya Hong Kong na Makau
pamoja na sehemu ya Taiwan
na ya nchi mbalimbali duniani,
na kuhimiza ushirikiano katika
sekta za uchumi, teknolojia
na biashara.
Mwenyekiti wa sasa wa shirikisho
hilo ni Bwana Huang Mengfu.
|