Mapango ya Maijishan na Mapango ya Longmen
Radio China Kimataifa

Mapango ya Maijishan yako katika sehemu ya kaskazini magharibi ya China, mkoani Gansu. Kutokana na maandishi ya historia, mapango hayo yalianza kuchongwa katika karne ya 3 K.K. yaani Enzi ya Qin, na tokea hapo sanamu za Buddha mbalimbali zilianza kuchongwa mlimani kuanzia mita 30 juu ya ardhi hadi mita 70.

  Sanamu za Buddha zilichongwa ndani ya mapango 194 yenye sanamu 7000, na jumla ya picha kwenye kuta za mapango zina mita za mraba 1300. Sanamu hizo na picha zinasaidia sana uchunguzi wa historia ya dini ya Buddha, historia, mila na desturi za raia.

Mapango ya Longmen yako katika mkoa wa Henan, karibu na mji mkuu wa mkoa huo kwa kilomita 13. mapango kwa jumla yako 2300 na sanamu za Buddha zaidi la lakini moja, na kuna mawe yenye maandishi 3600, minara ya dini ya Buddha 40. ndani ya mapango kwenye kuta pia kuna picha za kuchorwa.

 Sanamu na picha hizo ni vitu halisi kwa ajili ya utafiti wa enzi za kale za China Kati ya mapango hayo, pango moja linaloitwa Pango la Binyang lilianza kuchongwa mwaka 500 na kumalizika mwaka 523. Sanamu ya Buddha ndani ya pango hilo pamoja na wafuasi wake zote zilichongwa kama watu wa kweli, hata mikunjo ya nguo inaonekana wazi.