Magofu ya Yin na Maneno kwenye Gamba la Kobe
Radio China Kimataifa

Kwa sababu historia ya China ina karne kadhaa, vitu vya utamaduni vilivyoko chini ya ardhi ni vingi. Tokea karne ya 20 teknolojia ya kisasa ya nchi za Magharibi ilipoanza kutumika nchini China, vitu vingi vya kale viligunduliwa.

Mjini Anyang mkoani Henan, kuna magofu yenye kilomita za mraba 24. Hayo ni magofu maarufu ya Yin. Kutokana na maandishi ya historia, katika karne 14 K.K. mfalme wa Enzi ya Shang alihamisha mji mkuu kutoka mji wa Qubu hadi Anyang, tokea hapo katika miaka 300, mji huo ulikuwa ni mji mkuu wa Enzi ya Shang. Mwaka 1046 K.K. mfalme wa Enzi ya Zhou alimshinda mfalme wa Enzi ya Shang, mji huo ukawa magofu. Kwa sababu Enzi ya Shang pia inaitwa Enzi ya Yin, kwa hiyo magofu hayo yamepewa jina la "Magofu ya Yin".

Magofu ya Yin ni ugunduzi mkubwa wa vitu vya kale katika karne ya 20 nchini China. Mwaka 1928 katika ugunduzi mwa mwanzo yaligunduliwa maneno kwenye gamba la kobe, vyombo vya shaba nyeusi.

 Maneno kwenye gamba la kobe yalitumika kwa ajili ya kupiga ramli, kwenye gamba hilo yalichongwa majina ya wapiga ramli, tarehe na maswali yaliyoulizwa, kisha kukaushwa kwa moto na gamba likapasuka. Wapiga ramli watapata majibu kutokana na mipasuko.

Hivi sasa kuna magamba kama hayo laki moja na elfu 60, na kati ya magamba hayo baadhi ni vipande tu ambavyo havina maandishi, kutokana na hesabu, maneno kwenye magamba ni zaidi ya elfu nne, na kati ya maneno hayo elfu nne yaliyotambulika kwa maana yake yako zaidi ya elfu moja. Kutokana na maneno hayo elfu moja, watu wa leo wanaweza kufahamu kwa kiasi fulani hali ya siasa, uchumi na utamaduni katika Enzi ya Shang.

Mtaalamu mashuhuri Bw. Guo Muore aliandika matokeo yake ya utafiti wa maneno kwenye gamba la kobe mwaka 1929. hivi sasa wataalamu wa maneno hayo ni profesa Qiu Sigui wa Chuo Kikuu cha Beijing na profesa Li Xueqin wa Taasisi ya Historia ya China.

Magamba ya kobe yenye maneno licha ya kugunduliwa katika magofu ya Enzi ya Shang, mengine ambayo yalikuwa mapema zaidi ya Enzi ya Zhou Magharibi pia yaligunduliwa, lakini magamba hayo hayana maneno mengi. Katika muda wa miaka 70 iliyopita, wataalamu wa mambo ya kale wamegundua mahekalu zaidi 50, makaburi 12 na makaburi mengi ya makabwera na matajiri na vyombo vya udongo, vyombo vya shaba nyeusi katika magofu ya Enzi ya Shang. Vitu hivyo vimewafahamisha watu kimsingi hali ya jamii ya kale nchini China.