Hekalu la Famensi
Radio China Kimataifa

Hekalu la Famensi liko katika mkoa wa Shanxi, magharibi mwa China, hili ni hekalu maarufu sana kwa sababu ndani ya hekalu hili chini ya pagoda kilizikwa kipande cha mifupa ya mwanzilishi wa dini ya Buddha, Sakyamuni. Aprili, mwaka 1987, watalamu wa mambo ya kale walipojenga upya pagoda ya Buddha lililoporomoka, bila makusudi waligundua ukumbi mmoja ulio chini ya msingi wa pagoda ya zamani, vitu ndani ya ukumbi huo vilistaajabisha duniani. Ugunduzi wake unathaminiwa kama ugunduzi wa sanamu za askari na farasi za Enzi ya Qin.

Hekalu la Famensi liko mbali na mji wa Xi An kwa kilomita 120 upande wa magharibi, lilijengwa katika Enzi ya Wei Kaskazini nchini China, yaani mwaka 499 hivi. Hekalu hili liliwahi kuwa na ustawi mkubwa katika Enzi ya Tang iliyokuwa katika karne ya 7 nchini China. Serikali ya Enzi ya Tanga ilitumia pesa nyingi na watu wengi kuongeza majengo katika hekalu hilo mpaka likawa na nyua 24 za nyumba, na watawa elfu 5. Wakati huo hekalu hili lilikuwa kubwa kabisa katika eneo la mji mkuu wa Enzi ya Tang.

Kutokana na vidokezo vya dini ya Buddha, ili kuenzi dini ya Buddha mfalme mmoja wa India ya kale ambaye aliifanya dini hiyo iwe ya kitaifa aliigawa mifupa ya mwanzilishi wa dini ya Buddha, Sakyamuni, kwa vipande vipande na kuvizika chini ya pagoda 84,000 duniani. Pagoda kama hizo 19 zilijengwa nchini China, na pagoda ndani ya hekalu la Famensi ni moja kati ya hizo.

Kwa sababu ya kuzikwa kipande cha mfupa wa mwanzilishi wa dini ya Buddha, hekalu hilo lilipata waumini wengi na umaarufu duniani. Kutokana na vitabu vya zamani, jumla walikuwako wafalme wanane wa Enzi ya Tang waliwahi kuchukua sehemu ya mwili wa Sakyamuni hadi kwenye kasri ya kifalme na kuabudu, na walitoa zawadi nyingi kwa hekalu hilo. Lakini kutokana na vita, mitetemeko ya ardhi, hali ya ustawi wa hekalu hilo baadaye ukatoweka kabisa.

Mwaka 1981, pagoda yenye matabaka 13 iliporomoka kutokana na mvua. Mwaka 1987, mkoa wa Shanxi ulishirikisha wataalamu wa mambo ya kale kufanya uchunguzi juu ya msingi uliobaki wa pagoda, na wakagundua ukumbi huo uliokuwa chini ya ardhi kwa miaka 1,113. Eneo la ukumbi huo ni mita za mraba 31.48, ndani yake vilikuwako vitu vingi vya Enzi ya Tang, licha ya kipande cha mfupa wa Sakyamuni, pia viko vyombo vya kauri, vitambaa vya hariri vya Enzi ya Tang. Kwa mujibu wa takwimu za historia, vitambaa vya hariri vilivyoko ndani ya ukumbi huo ni vya hali ya juu. Uzi wa dhahabu wa kushonea una unene wa milimita 0.1 na ulio mwembamba sana una milimita 0.66 tu ambao ni mwembamba kuliko unywele. Ndani ya sanduku lililosukwa kwa matawi ya miti kiliwekwa kitambaa cha hariri, ingawa unene wa kitambaa chenyewe kilichokunjuka una sentimita 23 tu lakini kina matabaka 780.

Ndani ya ukumbi huo pia zimegunduliwa vyombo vingi vya dhahabu na fedha, na vya kauri.

Ili kutunza hekalu na vitu vyake vilivyochimbuliwa, yamejengwa makumbusho. Kwa kushirikiana na wataalamu wa Ujerumani, wataalamu wa China wamefankiwa kupata teknolojia ya juu kuhifadhi vitabaa vya hariri. Mwaka 2002 kipande cha mfupa wa mwanzilishi wa dini ya Buddha, Sakyamuni, kilipelekwa Taiwan kwa makusudi ya kuabudiwa. Katika muda wa mwezi mmoja, waumini waliokwenda kuabudu walifikia milioni 4.