Utamaduni wa Sanxingdui
Radio China Kimataifa

China ina ardhi kubwa na ilipokuwa katika zama za kale, kulikuwa na madola mengi madogo madogo. Mkoa wa sasa wa Sichuan ulikuwa ni Dola la Shu lililopo. Katika miaka ya 70 ya karne iliyopita, vitu vilivyofukuliwa katika Sanxingdui mkoani humo vilishangaza watu wa dunia. Mwaka 1986 wataalamu wa mambo ya kale waligundua mashimo makubwa mawili yaliyozikwa vitu vya thamani kubwa zaidi ya 1000 kwa ajili ya tambiko. Vitu vya utamaduni ambavyo vilikuwa vimelala kwa miaka 3000 chini ya ardhi vimefukuliwa.

Ndani ya vitu vilivyogunduliwa, vitu vya ajabu vilikuwa ni vinyago vya kuvaa usoni vya shaba nyeusi, vinyago hivyo karibu vyote vina njusi nene, macho makubwa, mgongo wa pua ulioinuka sana, mdomo mpana na kutokuwa na kidevu. Uso unaonekana si kama kucheka wala kukasirika. Sura za vinyago zilitofautiana sana na sura halisi za watu wa zama zile, lakini sura za vinyago zinamaanisha nini?

Katika mashimo hayo mwaili pia iligunduliwa sanamu ya mwili mzima ya shaba nyeusi. Sanamu hiyo ina kimo cha sentimita 170, ni sanamu kubwa kabisa ya shaba nyeusi duniani. Wataalamju wanaona kuwa Sanamu hiyo ilionekana si ya mtu wa kawaida, na iligunduliwa katika shimo la kufanyia tambiko.

Licha ya vinyago na sanamu, pia viligunduliwa vitu vingi vya bakora ya dhahabu, meno ya ndovu na "mti wa ajabu". Bakora ya dhahabu ina urefu wa mita 1.42, juu yake kuna michoro na ndege wawili na samaki wawili. "mti wa ajabu" una urefu wa mita nne na una matawi tisa katika matabaka matatu, na kwenye kila tawi alisimama ndege mmoja. Kutokana na utafiti, ndege hao haimaanishi ndege wa kawaida, bali ni ndege wa mungu wanaowakilisha jua.

Wataalamu wamegundua kuwa vitu vilivyofukuliwa vina mtindo wa Dola la Shu lakini pia vina mtindo wa Misri, na vikombe vya mvinyo vina mtindo wa Kimagharibi. Hii ikimaaisha kuwa Dola la Shu lilikuwa na mawasiliano na nchi za nje.