Kaburi la Mfalme Zhu Yuanzhang I
Radio China Kimataifa

Kaburi la Mababu wa Enzi ya Ming lilikuwa ni kaburi lililojengwa na mwanzilishi wa Enzi ya Ming, Zhu Yuanzhang, kwa ajili ya mababu zake, ni kaburi la kwanza kabisa katika Enzi ya Ming (1368-1644). Zhu Yuanzhang alizaliwa mwaka 1368 katika ukoo maskini vijijini na kufa mwaka 1398. Ili asilale na njaa, aliwahi kuwa sufii katika hekalu fulani. Baadaye alishiriki katika uasi wa wakulima ulioanzia mwaka 1271 hadi 1368. Kwa sababu ya uhodari na ujasiri wake katika mapambano hatua kwa hatua akawa kiongozi wa waasi kutoka askari wa kawaida, na mwishowe mwaka 1368 alikuwa mfalme wa enzi yake ya Ming.

Baada ya Zhu Yuanzhang kuwa mfalme alijenga kaburi kwa ajili ya babu yake, baba wa babu yake na babu wa babu yake, alizika nguo na kofia za watu hao ndani ya kaburi.

Kaburi hilo liko kando ya Ziwa la Hongze, ambalo ni moja kati ya maziwa makubwa manne ya maji baridi nchini China. Kaburi hilo lilijengwa kwa miaka 28. kutokana na maandishi ya historia, katika sehemu ya kaburi kuna kuta za tabaka tatu za kuizungukia sehemu ya kaburi, madaraja matatu, kumbi, vibanda na nyumba, kwa jumla kuna vyumba karibu elfu moja. Mpaka sasa kuna barabara ya kufikia kwenye kaburi, barabara hiyo ina urefu wa mita 250 kutoka kusini hadi kaskazini, na pembeni mwa barabara kuna sanamu za wanyama na maofisa, jumla ya sanamu hizo ni 42 ambazo mbili mbili zinakalibiana pande mbili za barabara.

Mwaka 1680 kaburi hilo lilizama ndani ya ziwa kutokana na mafuriko makubwa. Mwaka 1963 sehemu ya ziwa la Hongze ilipata ukame, sanamu nyingi zilionekana, sanamu hizo kila moja ina kimo cha mita zaidi 3 na uzito tani 10. kumbi ziliporomoka, lakini kutokana na uchunguzi, wataalamu wamethibitisha kuwa vitu vingi ndani ya kaburi havijaharibika.

Baada ya ukame uliotokea mwaka 1963, ukame mwingine pia ulitokea mwaka 1993, na 2001. Hasa ukame uliotokea mwaka 2001 ukuta wa ulionekana kwa sehemu kubwa kuliko miaka yote iliyokuwa na ukame. Ingawa majengo juu ya ardhi yameharibika, lakini ukubwa na ufahari wa kaburi hilo bado unaonekana wazi.