Kaburi la Mababu wa Enzi ya Ming II
Radio China Kimataifa

Kaburi la mfalme wa kwanza wa Enzi ya Ming (1368-1644), Zhu Yuanzhang ni moja ya makaburi makubwa ya kale duniani.

Zhu Yuanzhang alizaliwa mwaka 1368 katika ukoo maskini vijijini na kufa mwaka 1398. Ili asilale na njaa, aliwahi kuwa sufii katika hekalu fulani. Baadaye alishiriki katika uasi wa wakulima ulioanzia mwaka 1271 hadi 1368. Kwa sababu ya uhodari na ujasiri wake katika mapambano hatua kwa hatua akawa kiogozi wa waasi kutoka askari wa kawaida, na mwishowe mwaka 1368 alikuwa mfalme wa enzi yake ya Ming.

Kaburi la mfalme huyo Zhu Yuanzhang lilianza kujengwa katika miaka alipokuwa mfalme na lilimalizika baada ya mtoto wake kurithi kiti chake cha ufalme, jumla lilitumia miaka 25. Kwa kuwa mwanzoni Zhu Yuanzhang aliufanya mji wa Nanjing kuwa mji mkuu, kaburi lake lilijengwa huko, lakini baadaye mtoto wake alichagua Beijing kuwa mji mkuu. Kwa hiyo, miongoni mwa makaburi ya wafalme wa Enzi ya Ming, ni kaburi hilo tu lililojengwa kaika Nanjing, mengine yote yalijengwa kwenye vitongoji vya Beijing. Ukuta wa kuzunguka kaburi la Zhu Yuanzhang una urefu wa kilomita 22.5 ambao ni sawa na thuluthi mbili ya urefu wa ukuta wa mji wa Beijing. Kutokana na uharibifu wa hali ya hewa katika miaka mia sita, mbao zote za majengo kwenye sehemu za kaburi ziliozwa, lakini hata hivyo kutokana na misingi ya mawe ukubwa wa majengo unaweza kuonekana wazi. Mtindo wa majengo unafanana na ule wa makaburi mengine ya wafalme wa Enzi ya Ming ila eleo lake ni kubwa zaidi. Kwa hiyo ni wazi kwamba makaburi ya wafalme wengine wa Enzi ya Ming yaliyojengwa katika Beijing yote yaliiga mtindo wa kaburi hilo la mfalme wa kwanza wa enzi hiyo, Zhu Yuanzhang.

Tofauti na maburi mengine ya Enzi ya Ming ni kuwa njia ya kufikia kaburi ni njia ya kupindapinda badala ya kunyooka. Baadhi wanasema kwamba Zhu Yuanzhang alitaka kujionyesha wazo lake tofauti na wengine katika ujenzi wa makaburi, baadhi wanasema kuifanya njia iwe ya kupindapinda ni kwa ajili ya kurefusha njia ya kufikia kaburi. Njia hiyo ilianza kutoka kibanda kikubwa chenye jiwe la kaburi, paa la kibanda hicho limeharibika kabisa, zilizobaki sasa ni kuta nne tu. Ndani ya kibanda hicho kuna jiwe refu kubwa lenye maandishi yaliyoandikwa na mtoto wake, yakieleza sifa za baba yake Zhu Yuanzhang, jumla maneno 2746. Kwenye sehemu ya kati ya njia, pande mbili zilipangwa sanamu za wanyama wawili wawili sawa kukabiliana, sanamu hizo ni za simba, ngamia, ndovu, farasi n.k., jumla aina 12 na kwenye njia inayoelekea kaskazini zilipangwa sanamu za maofisa na askari zenye ukubwa kama kitu halisi.

Mfalme Zhu Yuanzhang alizikwa pamoja na mkewe katika ukumbi ulio chini ya ardhi. Kuhusu mahali ukumbi huo ulipo watu walikuwa na mawazo tofauti. Ili kuzuia wizi wa mali za kaburini, mazishi yalifanywa kwa ujanja kutoka milango yote 13 ya mji kwa wakati mmoja, na mazishi yote yalikuwa sawa ili kubabaisha ya kweli, kwa hiyo wapi maiti ya mfalme Zhu Yuanzhang ilipo ilikuwa fumbo katika miaka mingi. Kuanzia mwaka 1997, wataalamu wa mambo ya kale walifanya uchunguzi mara nyingi kwa teknolojia ya juu katika eleo la mita 20,000, wakapata data zaidi ya 20,000, na wishowe wamehakikisha ukumbi ulipo wenye maiti ya mfalme. Wataalamu wa kusimamia ukaguzi huo wanasema kwamba ukumbi wa maiti ya Zhu Yuanzhang uko chini ardhi kwa mita kumi kadhaa, na ukumbi huo uko salama bali haukuwahi kuibiwa kama uvumi ulivyosemwa miaka mingi.

Kulingana na makaburi ya wafalme waliotangulia, handaki lililochimbwa chini ya ardhi la kupeleka jeneza ukumbini licha ya kutonyooka tena linaachana na mstari wa kulenga ukumbi moja kwa moja, sababu yake haifahamiki hadi leo. Mtindo huo pia uliigwa na wafalme waliofuata wa Enzi ya Ming katika ujenzi wa makaburi yao. Kwa mfano, kaburi la Ding lililokuwa limechimbuliwa miongoni mwa makaburi 13 ya wafalme wa Enzi ya Ming katika vitongoji vya Beijing, handaki lake la kupeleka jeneza kwenye ukumbi wa maiti liliachana na ukumbi kwa upande wa kushoto, kinyume na kaburi la Zhu Yuanzhang. Kadhalika, wataalamu wa mambo ya kale wamegundua kwamba juu ya kilima cha kaburi sehemu kiasi cha 60% hivi ilijengwa kwa mikono, yaani kwenye sehemu hiyo yalipangwa mawe makubwa mengi. Kutokana na uchunguzi, mawe hayo hapo awali yalikuwa chini ya kilima, mawe hayo licha ya kutia uzuri wa kilima cha kaburi hilo, tena yanaweza kuzuia mmomonyoko wa udongo na wizi wa kaburi. Kitu cha ajabu ni kwamba wataalamu wa mambo ya kale wamegundua kumbe sanamu za wanyama zote zilichongwa kwa visukuku vya viumbe vilivyokuwa na miaka milioni 300 iliyopita, na baadhi hata vinaweza kuonekana kwa macho na baadhi vinaweza kuonekana kwa kusaidiwa na kioookuzi. Kutokana na ugunduzi huo, sanamu hizo licha ya kuwa na thamani ya kihistoria, kisanaa tena zina thamani kubwa za kisayansi.