Makaburi 13 ya Enzi ya Ming
Radio China Kimataifa

Zhu Yuanzhang, mfalme wa kwanza wa Enzi ya Ming, aliufanya mji wa Nanjing kuwa mji mkuu, alipokufa alimrithisha kiti cha enzi yake mjukuu wake badala ya wanawe. Kutokana na hayo mtoto wake wa nne, Zhu Li alizusha vita kutaka kunyakua utawala wa enzi hiyo, na mwishowe alifanikiwa. Alipouteka mji mkuu Nanjing, yule mjukuu aliyerithishwa ufalme alikuwa ametoroka na hakujulikana wapi alikokwenda, hadi sasa suala hili bado ni fumbo. Baada ya kushika utawala, Zhu Li aliona kwamba mji wa Nanjing ulikuwa si salama, akauacha Nanjing na kufanya Beijing kuwa mji mkuu. Mfalme Zhu Li alianza kujenga kaburi lake alipokuwa katika utawala wake. Baada ya kuchunguza chunguza mwishowe aliamua sehemu ya magharibi viungani mwa Beijing kujenga kaburi lake. Hapo ni sehemu yenye mandhari nzuri na milima ya kijani, akalipatia kaburi lake jina la "Kaburi la Chang Ling". Toka mwaka 1409 kaburi la Zhu Li lilipoanza kujengwa hadi 1644 Enzi ya Ming ilipomalizika, katika miaka zaidi ya 200, jumla wafalme 13 wa Enzi ya Ming walizikwa katika sehemu hiyo.

Ni kama mpangilio wa ujenziwa kaburi la mfalme wa kwanza wa Enzi ya Ming, Zhu Yuanzhang, kwamba katikati ya sehemu ya makaburi 13 kuna njia ya kupeleka jeneza. Mbele ya lango kuu la sehemu kya makaburi kuna mlango mkubwa wa uliogengnezwa kwa mawe tupu ya marumaru, hadi leo mlango huo umekuwa na miaka 450. Baada ya kupita mlango huo kuna lango kuu la sehemu ya makaburi. Hili ni lango ambalo mfalme lazima alipite alipokwenda kutambika. Kuanzia pande mbili za lango hili ulijengwa ukuta wenye kilomita 40 uliozunguka sehemu ya makaburi mlimani. Ukuta huo una vipito 10 licha ya lango kuu. Nyakati zile kila kipito kilikuwa kikilindwa na askari wengi ili kuhakikisha usalama wa shemeu ya makaburi. Katika sehmu ya makaburi, kulikuwa na nyumba za wasimamizi, ambao kazi yao ni kushughulika na mambo ya kutoa heshima kwa marehemu:kuna nyumba za watunza bustani ambao kazi yao ilikuwa ni kushughulika za tambiko, na nyumba za walinzi ambao kazi yao ni kulinda sehemu ya makaburi.

Kwa ajili ya kuhifadhi kaburi lisiibiwe, wafalme licha ya kubuni hadithi nyingi za kuwatisha wezi wa mali ya makaburi, nao pia walificha sana makaburi yao yenyewe. Kwa hiyo ilikuwa ni vigumu kuupata ukumbi wa kuwekea maiti ndani ya kaburi la Ding Ling ulikuwa haujulikani, na haukujulikana mpaka mwezi Mei mwaka 1956 wataalamu wa mambo ya kale walipoanza kulichimbua kaburi hilo. Kutokana na juhudi hatimaye waligundua kaburi. Ukumbi wa kuwekea maiti ndani ya kaburi la Ding Ling una mita za mraba 1195 ambao umegawanyika katika sehemu tano, yaani ya mbele, ya kati, ya nyuma, ya kulia na kushoto. Ukumbi huo ulijengwa kwa mawe matupu. Mbao zilitandikwa sakafuni ili gari la kubeba jeneza lilipoingia ndani ya ukumbi huo lisiharibu sakafu, mbao hizo mpaka sasa bado zipo. Katikati ya ukumbi huo kuna viti vitatu vya mawe vinavyoashiria madaraka, sehemu ya nyuma ya ukumbi huo ni muhimu, kwani katika sehemu hiyo jukwaani yamewekwa majeneza matatu. Kati ya majeneza hayo matatu, la katikati ni kubwa zaidi ambalo ni la mfalme, mengine mawili pembeni ni majeneza ya malkia wawili. Pembeni kuna masanduku 26 ya kafara na majagi makubwa ya kauri. Kutoka katika kaburi la Ding Ling vimepatikana vitu vya utamaduni zaidi ya 3000, miongoni mwa vitu hivyo, kuna vitambaa vya hariri, nguo, mapambo na vyombo vya dhahabu na vya kauri ambavyo vyote vina thamani kubwa katika kufanya uchunguzi wa sanaa za Enzi ya Ming.