Kaburi la Enzi ya Han kwenye Mawangdui
Radio China Kimataifa

          

Katika miaka ya 70 kaburi moja la Enzi ya Han lililopo kwenye Mawangdui mjini Changsha liligunduliwa. Kaburi lilo lilishangaza dunia nzima kwa maiti iliyopatikana ndani ya kaburi ni maiti pekee duniani yenye miaka 2000 bila kukauka. Pamoja na maiti pia vilifukuliwa vitu vingi vya thamani.

Miaka mingi wenyeji wa mji wa Changsha walikuwa wanasimulia kuwa huko kuna kaburi la kale, lakini kaburi hilo halikuthibitishwa mpaka mwaka 1971. watu walitoboa tundu kwa mtarimbo chini ya ardhi kwa zaidi ya mita kumi, hewa iliyotoka kutoka tundu inapalia pua, na iliwaka kwa kibiriti bila kuzimika.

Jeneza ilifungwa kwa matope meupe ya jasi yenye unene wa mita moja na baada ya matope ni sehemu ya makaa yenye uzito kiasi ya kilo 5000. Jeneza lina matabaka manne, na tabaka la nje lina urefu karibu mita 7, upana mita 5 na kimo mita 3.

Baada ya kufumua jeneza, ndani yake ni maiti ya mwanamke ambayo haujakauka, ngozi bado laini, mikono na miguu inaweza kupindika, na hata alama za vidola vya mikono na miguu inaonekana wazi. Kwa uchunguzi, mwanamke huyo alizikwa katika karne ya pili K.K. yaani mwanzoni mwa Han Magharibi.

Ugunduzi wa "maiti ya mwanamke yenye miaka elfu mbili bila kuoza" ulishangaza dunia nzima. Wataalamu, watalii, wapiga picha walimiminikia mjini Changsha. Pamoja na maiti, pia viligunduliwa vitu vingi vya vitambaa vya hariri, vyakula, dawa, sanamu za mbao, ala za muziki. Kati ya vitu hivyo, vitambaa vya hariri vilikuwa vingi na vilisifiwa kuwa ni "ghala kubwa la hariri la Han Magharibi (206 K.K.- 25 K.K.)".

Ugunduzi wa kaburi la Mawangdui umetoa mchango mkubwa, hasa maiti iliyokamilika na vibao vyenye maandishi. Kwa hiyo ugunduzi huo unasifiwa kuwa ni "ugunduzi mkubwa duniani katika karne ya 20".