Nyongeza kuhusu Vtu Vlivyofukuliwa katika Kaburi la Mfalme Qinshihuang
Radio China Kimataifa

Miaka sita baada ya kugundua sanamu za askari na farasi katika kaburi la mfalme wa kwanza wa Enzi ya Qin, Qinshuhuang, mwaka 1980 wataalamu wa mambo ya kale waligundua farasi na mkokoteni wa shaba.

Vitu hivyo viligunduliwa na mtaalamu wa mambo ya kale Yang Xude kwenye mahali palipo chini ya ardhi kwa mita 7.

Kwa kuelekezwa na wataalamu wa mambo ya kale, waanyakazi walichimba kwa makini, walitumia kiasi cha mwezi mmoja mwishowe walipata mikokoteni miwili, farasi wanane, na mikono miwili ambayo yote ni ya shaba kwenye mahali palipo chini ya ardhi kwa mita 7.8.

Vitu hivyo vilichukuliwa pamoja na udongo wenye ujazo wa mita moja kwa kufungwa na mbao na kisha kuchukuliwa kwa winchi, na baada ya kupelekwa kwenye jumbo la maonesho wataalamu wa mambo ya kale walitumia karibu miaka miwili kuzisafisha sanamu hizo kabla ya kuzionesha hadharani.

Sanamu za mikokoteni na farasi ni nusu ya vitu vya kweli, lakini namna ya kutengeneza sanamu hizo zilikuwa ni fumbo.