Kitambaa cha Mabegani
中国国际广播电台
 

      Kitambaa cha mabegani kilianzia Enzi ya Sui (581-618) na ilipofika Enzi ya Qing (1644-1911) kitambaa hicho kilikuwa pambo, hasa kwa wanawake. Kitambaa hicho kinatariziwa kwa muda mrefu, na picha kwenye kitambaa hicho huwa ni maua, ndege au watu katika hadithi za mapokeo. Kitambaa cha mabegani katika picha ni cha mkoa wa Henan, picha iliyotariziwa ni mawingu, maua na ndege na watu na daraja.