Kinanda Leiqin
中国国际广播电台

    Leiqin ni kinanda kilichotokea katika miaka ya 20 ya karne ya 20.

Kinanda hicho kilibuniwa na mwanamuziki Wang Diayu. Wang Dianyu alikuwa mkazi wa Mkoa wa Shandong, familia yake ilikuwa maskini na alikuwa mlemavu wa macho. Mwishoni mwa miaka ya 20 ya karne ya 20 alibuni kinanda hicho na katika mwaka 1953 kinanda hicho kilipewa jina la Lieqin .

Leiqin ni kama kinanda Erhu , ina nyuzi mbili za chuma cha pua, kinanda hicho kikubwa kina urefu wa sentimita 110 na kidogo kina urefu wa sentimita 90.

Mpigaji wa kinanda hicho anatumia mkono wa kushoto kurekebisha sauti na kuvuta upinde kwa mkono wa kushoto.

Leiqin ina eneo kubwa la sauti na sauti yake pia ni kubwa, inaweza kuchezwa peke yake na pia kushirikiana na bendi na inaweza kuiga sauti ya binadamu.

Mnasikiliza : Wimbo wa Afanti