Xun
中国国际广播电台

      Xun ni ala ya muziki kwa kupulizwa, imekuwa na historia ya milenia nchini China.

Hapo awali, Xun ilikuwa donge la udongo au la mawe lililofungwa kamba kwa ajili ya kuua ndege na wanyama. Baadhi ya madonge yalikuwa na matundu, na yaliporushwa yalikuwa yanalia, baadaye watu walitumia kama ni ala ya muziki.

 

  Hatimaye ala hiyo ilitengenezwa kwa vigae, kwa maumbo ya duara, samaki na tunda la pea. Mwanzoni ala hiyo ilikuwa na tundu moja tu, hadi mwishoni mwa karne ya tatu ala hiyo ilikuwa na matundu sita.

Mwishoni mwa miaka ya 30 ya karne ya 20 wanamuziki walivumbua Xun yenye vitundu tisa. Ala hiyo inafaa kuonesha hisia ya huzuni.

Tokea Xun kuwa na vitundu tisa, ala hiyo imekuwa muhimu katika ala za muziki za Kichina.

Katika miaka ya karibuni wanamuziki waliendeleza ala hiyo kuwa na vitundu kumi. Hivyo eneo lake la sauti limekuwa kubwa zaidi.

Katika historia, Xun ilitumika zaidi katika muziki uliopigwa ndani ya kasri la kifalme. Kuna aina mbili za Xun ambazo zinatofautiana kwa ukubwa. Xun ndogo ina ukubwa kiasi cha yai, sauti yake ni ya juu, na aina nyingine ni kubwa na sauti yake ni nene.

Mnasikiliza: Wimbo wa kale wa Dola la Chu