Sheng
中国国际广播电台

      Sheng ni ala ya muziki yenye miaka mingi nchini China.

Sheng iligunduliwa mwaka 1978 katika kaburi la zama za kale mkoani Hubei, Sheng hiyo imekuwa na miaka zaidi ya 2400, ambayo ni ya miaka mingi sana katika ugunduzi wa Sheng nchini China.

Sheng inaweza kufuatiliwa mpaka miaka 3000 iliyopita. Hapo mwanzo Sheng ilikuwa ni paipu kadhaa zinapangwa kwa pamoja na kutoa sauti kwa kupuliza vitundu, baadaye watu walitia kilimi, yaani kipande kidogo chembamba kinachotoa sauti kwa kupulizwa.

Sheng ina paipu zaidi ya kumi na kufungwa kwa umbo la kwato la farasi.

Baada ya Jamhuri ya Watu wa China kuasisiwa, wanamuziki walifanya mageuzi na kuifanya ala hiyo kuwa na eneo kubwa la sauti.

Sheng ni ala muhimu katika bendi ya muziki wa Kichina. Kuna aina tatu za Sheng kutokana na ukubwa na tofatu za sauti.

Mnasikiliza:Phenix anayeruka angani