Chen Zuohuang
中国国际广播电台

Bw. Chen Zuohuang alizaliwa katika mji wa Shanghai, na alimaliza masomo yake ya uongozaji wa bendi mwaka 1981 katika chuo cha muziki cha taifa. Mwaka 1981 kutokana na mwaliko wa Bw. Seiji Ozawa alikwenda kusoma katika Tanglewood Music Centre na chuo cha muziki cha Michigan nchini Marekani, alipata shahada ya udaktari kwenye sanaa ya uongozaji bendi.

Tokea mwaka 1885 hadi mwaka 1987, Bw. Chen Zuohuang alikuwa naibu profesa wa uongozaji wa bendi katika chuo cha Kansas nchini Marekani, na alipata hadi ya udaktari. Mwaka 1987 Bw. Chen Zuohuang alikuwa mwongozaji wa bendi ya taifa, aliongoza bendi hiyo kufanya maonesho ya muziki katika miji 24 ya Marekani ikiwemo New York na Washington, ambapo walisifiwa na wasikilizaji na waongozaji wa bendi.

Kati ya mwaka 1990 na mwaka 2000 Bw. Chen Zuohuang alialikwa kuwa msimamizi mkuu na mwongozaji wa bendi ya The Witchita Symphony Orchestra. Kati ya mwaka 1992 na mwaka 1996 Bw. Chen alifanya kazi hiyo hiyo katika bendi ya Rhode Island Philharmonic Orchestra.

Bw. Chen Zuohuang alialikwa kuwa mwongozaji wa bendi katika nchi na sehemu zaidi ya 20 zikiwemo za The Zurich Tonhalle Orchestra na Vancouver Symphony Orchestra. Ustadi wa uongozaji bendi unasifiwa na wasikilizaji na waongozaji wa muziki kuwa mwanamuziki hodari sana.

Mwaka 1996 Bw. Chen Zuohuang aliacha kazi alizofanya katika nchi za nje na kurejea nchini. Alianzisha kundi la Symphony Orchestra ya China na kuwa msimamizi mkuu wa sanaa wa kundi hilo. Kundi hilo linafuata utaratibu wa maonesho ya majira ya muziki unaotekelezwa duniani, katika miaka michache iliyopita alialika wanamuziki hodari zaidi ya mia moja kufanya maonesho ya muziki nchini. Shughuli hizo zimechangia sana maendeleo ya muziki wa Symphony nchini.



  
  [Burudani za Muziki]Furaha Baada ya Mawio