Hali ya Jumla ya Miundo ya Uzalishaji

中国国际广播电台

       

 

Miundo ya uzalishaji ni uhusiano wa moja kwa moja wa uwiano na muundo wa vitu muhimu vya uzalishaji mali kati ya sekta mbalimbali za uzalishaji mali. Uhusiano huo hasa upo katika sekta tatu za uzalishaji mali za kilimo, viwanda na utoaji huduma pamoja na uhusiano wa uwiano ndani ya sekta hizo.

Tangu China mpya iasisiwe mwaka 1949, muundo wa sekta za uzalishaji mali ulipita katika vipindi vitatu vya maendeleo: Kipindi cha kwanza ni kati ya mwanzoni mwa miaka ya 50 ya karne iliyopita na mwishoni mwa miaka ya 70, ambapo China ilibadilisha hali ya uchumi wa nusu koloni na kuweka msingi wa viwanda. Kipindi cha pili ni kutoka mwaka 1979 hadi mwanzoni mwa miaka ya 90 ya karne iliyopita, China ilitekeleza sera za mageuzi na kufungua mlango kwa nje na kurekebisha miundo ya sekta za uzalishaji mali, ili kuiwezesha China kuingia kipindi cha kati cha maendeleo ya viwanda. Kipindi cha tatu ni kuanzia mwanzoni mwa miaka ya 90 ya karne iliyopita, China ilipoweka lengo la kujenga utaratibu wa uchumi wa kimasoko wa kiujamaa, hadi mwaka 2020, ambapo China licha ya kukamilisha ujenzi wa mambo ya viwanda, itafikia kwa hatua ya mwanzo mafanikio ya upashanaji habari.

Katika miaka zaidi ya 50 iliyopita, mabadiliko makubwa yametokea katika uhusiano wa uwiano kati ya sekta tatu za uzalishaji mali. Toka mwanzoni mwa miaka ya 50 ya karne iliyopita hadi mwaka 2002, shughuli za kilimo nchini China zilipungua kutoka 45.4% hadi 14.5%, shughuli za viwanda ziliongezeka kutoka 34.4% hadi 51.8%, na sekta ya utoaji huduma ilikuwa na ongezeko la 33.7% kutoka 20.2%.