Viwanda

中国国际广播电台

       

 

Maendeleo ya kasi ya viwanda vya China yalianza kutokea mwanzoni mwa miaka ya 50 ya karne iliyopita. Baada ya China mpya kuasisiwa mwaka 1949, viwanda vya China viliingia kipindi cha kufufuka na maendeleo. Hadi kabla ya kufanyika mageuzi mwaka 1978, China ilikuwa imejenga mfumo wa uchumi wa viwanda. Sekta ya kijadi ya uzalishaji wa mafuta ya asili ya petroli na viwanda vipya vya kemikali na elektroniki vilikuwa na maendeleo ya haraka, wakati viwanda vya nyuklia na usafiri kwenye anga ya juu ambavyo ni sekta ya uzalishaji mali ya sayansi na teknolojia ya kiwango cha juu, vilipata mafanikio makubwa. Tokea mwishoni mwa miaka ya 70 ya karne iliyopita, maendeleo ya viwanda vya China yaliimarishwa kwa hatua kubwa zaidi. Kati ya mwaka 1979 na mwaka 2003, wastani wa ongezeko la nyongeza ya thamani ya uzalishaji wa viwanda ulikuwa zaidi ya 10% kwa mwaka.

Kutokana na kuendelezwa kwa miaka zaidi 50 iliyopita, bidhaa muhimu za viwanda vya China ziliongezeka zaidi ya mara mamia kadhaa ambazo baadhi yake zinasafirishwa katika sehemu mbalimbali duniani. Toka mwaka 1996, uzalishaji wa chuma cha pua, makaa ya mawe, saruji, mbolea za chumvichumvi na televisheni umekuwa ukichukua nafasi ya kwanza duniani.

Mwaka 2003, nyongeza ya thamani ya uzalishaji wa viwanda ilikuwa Yuan za Renminbi trilioni 5 bilioni 361 na milioni 200, ikiwa ni ongezeko la 12.6% ikilinganishwa na ile ya mwaka uliotangulia. Hivi sasa, si kama tu kwamba China inaweza kuzalisha ndege, meli na magari, bali pia inaweza kuunda satellite ya dunia pamoja na zana za kisasa za viwanda. Hivi sasa China imekuwa na mfumo kamili wa viwanda. Katika siku za baadaye, China itatekeleza mkakati mpya wa kuleta maendeleo ya viwanda kwa teknolojia ya upashanaji wa habari na kuimarisha kuboresha viwanda kwa maenedeleo ya uchumi wa China.