Sekta ya Huduma

中国国际广播电台


      

 

Maendeleo ya haraka yalianza kutokea katika sekta ya huduma nchini China mwishoni mwa miaka ya 70 ya karne iliyopita.

Maendeleo hayo yalionekana hasa katika pande mbili: kwanza ni kupanuka kwa mfululizo kwa sekta ya huduma. Kutokana na takwimu, thamani ya ongezeko la sekta ya huduma nchini China kwa mwaka 2002 lilifikia Yuan za Renminbi trilioni 3 na bilioni 453.3 kutoka Yuan bilioni 86.05 mwaka 1978, ikiwa ni ongezeko la mara 39. Wastani wa ongezeko kwa mwaka ulikuwa zaidi ya 10%, kiasi hiki kilikuwa ni kikubwa zaidi kuliko jumla ya uzalishaji mali wa taifa nchini. Thamani ya ongezeko la sekta ya huduma katika jumla ya thamani ya uzalishaji mali kwa mwaka 2002 ilifikia 33.7%, kutoka 21.4% mwaka 1979. Mwaka 2003, japokuwa sekta ya huduma iliathiriwa vibaya na ugonjwa wa SARS na maafa ya kimaumbile ya ukosefu wa mvua na mafuriko, lakini bado kulikuwa na maendeleo ya kasi.

Kwa upande mwingine, sekta ya huduma nchini China ilikuwa njia muhimu ya kuongeza nafasi za ajira. Idadi ya watu wanaofanya kazi katika sekta ya huduma iliongezeka na kufikia zaidi ya milioni 210, ikiwa ni mara mbili kuliko ongezeko la wafanyakazi wapya katika sekta ya viwanda.

Hivi sasa, sekta ya huduma inahusiana na mambo ya migahawa, utalii, biashara rejareja ya bidhaa, sarafu, bima, upashaji wa habari, uchukuzi, matangazo ya biashara, sheria, uhasibu na utunzaji wa majengo ya wakazi. Kwa mujibu wa mpango wa maendeleo ya China, itakapofika mwaka 2020, ukubwa wa sekta ya huduma katika jumla ya uzalishaji mali wa nchini, utaongezeka kwa zaidi ya 50% kutoka kiasi cha theluthi moja ya hivi sasa.