|
|
|
|
|
Maeneo ya Ustawishaji wa
Uchumi Na Teknolojia
|
|
中国国际广播电台
Maeneo ya ustawishaji wa uchumi
na teknolojia ni moja ya sehemu
ya China inayofungua mlango
kwa nchi za nje. Kutenga eneo
dogo katika mji unaofungua mlango
kwa nje, kukamilisha ujenzi
wa miundo mbinu na mazingira
ya uwekezaji wa kiwango cha
kisasa duniani, ili kufanya
sehemu hiyo kuwa sehemu muhimu
katika uendelezaji wa uchumi
na biashara ya nje kwa mji huo
na kwa sehemu nyingine za karibu.
Mwaka 1988, baraza la serikali
liliidhinisha kuanzisha maeneo
ya ustawishaji wa uchumi na
teknolojia katika miji 14 ya
sehemu ya pwani ikiwa ni pamoja
na Dalian, Qinhuangdao, Tianjin,
Yantai, Qingdao, Lianyungang,
Nantong, Minhang, Hongqiao,
Chaohejing, Ningbo, Fuzhou,
Guangzhou na Zhanjiang. Hadi
sasa nchini China kuna maeneo
49 ya ustawishaji wa uchumi
na teknolojia ya ngazi ya taifa,
ambayo 27 yako katika sehemu
ya pwani ya mashariki na 22
yako katika sehemu ya magharibi
ya China. Aidha, baraza la serikali
liliidhinisha kutekelezwa sera
zinazotekelezwa katika maeneo
ya ustawishaji wa uchumi na
teknolojia ya ngazi ya taifa
katika maeneo mengine ya viwanda
na ustawishaji wa uchumi ya
Suzhou, Jinqiao, Ningbo, Xiamen,
Hainan na Yangpu.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|