Maeneo ya Ustawishaji wa Uchumi Na Teknolojia

中国国际广播电台


     
Maeneo ya ustawishaji wa uchumi na teknolojia ni moja ya sehemu ya China inayofungua mlango kwa nchi za nje. Kutenga eneo dogo katika mji unaofungua mlango kwa nje, kukamilisha ujenzi wa miundo mbinu na mazingira ya uwekezaji wa kiwango cha kisasa duniani, ili kufanya sehemu hiyo kuwa sehemu muhimu katika uendelezaji wa uchumi na biashara ya nje kwa mji huo na kwa sehemu nyingine za karibu.
Mwaka 1988, baraza la serikali liliidhinisha kuanzisha maeneo ya ustawishaji wa uchumi na teknolojia katika miji 14 ya sehemu ya pwani ikiwa ni pamoja na Dalian, Qinhuangdao, Tianjin, Yantai, Qingdao, Lianyungang, Nantong, Minhang, Hongqiao, Chaohejing, Ningbo, Fuzhou, Guangzhou na Zhanjiang. Hadi sasa nchini China kuna maeneo 49 ya ustawishaji wa uchumi na teknolojia ya ngazi ya taifa, ambayo 27 yako katika sehemu ya pwani ya mashariki na 22 yako katika sehemu ya magharibi ya China. Aidha, baraza la serikali liliidhinisha kutekelezwa sera zinazotekelezwa katika maeneo ya ustawishaji wa uchumi na teknolojia ya ngazi ya taifa katika maeneo mengine ya viwanda na ustawishaji wa uchumi ya Suzhou, Jinqiao, Ningbo, Xiamen, Hainan na Yangpu.