|
|
|
|
|
|
|
中国国际广播电台
China inatumia mitaji ya nchi
za nje kwa njia za aina mbalimbali,
ambazo kwa jumla zinaweza kugawanyika
katika mafungu matatu. Fungu
la kwanza ni kupata mikopo ya
nchi za nje, ikiwa ni pamoja
na kukopeshwa na serikali za
nchi za nje, mashirika ya fedha
duniani, benki za biashara za
nchi za nje na kutoa hati zenye
thamani za dhamana ya serikali
kwa nchi za nje. Fungu la pili,
kuwekezwa moja kwa moja na wafanyabiashara
wa kigeni, vikiwemo viwanda
vya ubia, vya ushirikiano na
vya wafanyabiashara wa kigeni;
Fungu la tatu ni uwekezaji wa
aina nyingine wa wafanyabiashara
wa kigeni, ambao ni pamoja na
ukodishaji, biashara yenye ruzuku,
kazi za usindikaji na uuzaji
wa hisa.
Kutoka mwaka 1990 hadi mwaka
2001, China ilitumia mitaji
ya nchi za nje dola za kimarekani
bilioni 510.8, ambayo ile iliyowekezwa
moja kwa moja na wafanyabiashara
wa kigeni ilikuwa dola za kimarekani
bilioni 378. Mitaji ya kigeni
iliyotumiwa na China mwaka 2002,
ilikuwa dola za kimarekani bilioni
55, ambayo ile iliyowekezwa
moja kwa moja na wafanyabiashara
wa kigeni ilikuwa dola za kimarekani
52.7, China ilichukua nafasi
ya kwanza katika kutumia mitaji
ya nchi za nje. Mwaka 2003,
uwekezaji wa wafanyabiashara
wa kigeni nchini China ulidumisha
ongezeko kubwa, ambapo kampuni
41,081 za wafanyabiashara wa
kigeni ziliidhinishwa kuanzishwa
nchini China, kiasi hiki kilikuwa
ni ongezeko la 20.2% kuliko
mwaka uliopita; Thamani ya mikataba
ya biashara iliyosainiwa ilikuwa
dola za kimarekani bilioni 115.1,
ambazo ni ongezeko la 39.0%;
Mitaji iliyotukika hasa ilikuwa
dola za kimarekani bilioni 53.5,
ikiwa ni ongezeko la 1.4%.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|