中国国际广播电台
Kampuni ya magari ya Volkswagen
ya Ujerumani katika miaka karibu
20 iliyopita, ilianzisha viwanda
viwili vya ubia vya magari katika
miji ya Shanghai na Changchun,
na baadhi ya viwanda vinavyozalisha
vipuri vya magari, pamoja na
mfumo wa vituo zaidi ya 100
vya vipuri vya magari.
Kiwanda cha Volkswagen cha Shanghai,
ambacho kiliwekezwa Yuan za
Renminbi zaidi ya bilioni 18.9,
hivi sasa kinazalisha magari
madogo namna miongo kadhaa ya
aina tano ambazo ni Santana,
Santana 2000, Passat, Polo na
Golf. Kiwanda cha magari cha
Changchun, ambacho kiliwekezwa
dola za kimarekani zaidi ya
Yuan bilioni 11.1, kinazalisha
magari ya nembo za aina mbili
za Audi na Volkswagen na aina
ya tano ya Audi A6. A4, Bora,
Jetta na Golf. Volkswagen imekuwa
kampuni kubwa kabisa ya magari
nchini China na kuwa na wateja
wengi kutokana na mabadiliko
ya aina za magari na huduma
bora.
Hivi leo, China imekuwa soko
la pili kwa ukubwa la Kampuni
ya Volkswagen duniani. Katika
muda wa miaka mitano ijayo,
kampuni hiyo itawekeza Euro
zaidi ya bilioni 5 nchini China.
BOEING
Kampuni ya Boeing imekuwa
na uhusiano mzuri wa Ushirikiano
na China toka mwaka 1972.
Kampuni ya Boeing inatoa mafunzo
nchini China kuhusu uendeshaji
na utunzaji wa ndege pamoja
na usimamizi ili kutoa dhamana
kwa shughuli za usafirishaji
wa ndege. Kampuni ya Boeing
imeanzisha mfumo wa huduma
za uwakilishaji uwanjani,
mahitaji na teknolojia nchini
China, na kusaidia Shirika
la Ndege la China kuinua kiwango
cha usimamizi wa mawasiliano
na usalama wa anga.
Aidha, Kampuni ya Boeing imekuwa
na ushirikiano mkubwa katika
uzalishaji na sekta ya uzalishaji
wa ndege nchini, na kujenga
viwanda vipya vya ubia vya
vifaa, marekebisho, utunzaji
na ukarabati wa ndege, pamoja
na kuanzisha shughuli za uuzaji
wa vipuli vya ndege.
Vipuri muhimu vya ndege za
Boeing 33,000 vinazotumika
hivi sasa, vilizalishwa nchini
China.
NOKIA
Kampuni ya Nokia ilianzisha
uhusiano wa kibiashara na
China tangu miaka ya 50 ya
karne iliyopita. Mwaka 1985,
kampuni ya Nokia ilianzisha
ofisi yake mjini Beijing.
Tokea katikati ya miaka ya
90 ya karne iliyopita, kampuni
hiyo ilijenga viwanda vya
ubia hapa China, na kuviendeleza
kuwa vituo vyake muhimu vya
uzalishaji duniani. Baada
ya kuingia karne mpya, Kampuni
ya Nokia ilishiriki zaidi
katika maendeleo ya sekta
ya teknolojia ya habari na
mawasiliano (IT) ya China
kwa kufanya ushirikiano na
sekta mpya ya teknolojia ya
upashanaji wa habari, na kujitahidi
kuiendeleza China kuwa kituo
chake cha kuandaa wataalamu
wa Kampuni ya Nokia.
Nchini China, Kampuni ya Nokia
imejenga vituo viwili vya
utafiti vya kilimwengu, kuanzisha
ofisi zake katika sehemu mbalimbali
na kuwa na wafanyakazi zaidi
ya 4,500. Bidhaa zote muhimu
za kampuni hiyo sasa zinazalishwa
hapa China, zikiwa ni pamoja
na simu mpya za mikononi,
vituo vya upashanaji wa habari,
mitambo ya udhibiti ya vituo,
kituo cha kubadilishana mawimbi,
zana za kupokea mawimbi, zana
za ubadilishanaji wa tarakimu
na simu zenye uwezo wa aina
nyingi.
MICROSOFT
Kampuni ya Microsoft iliingia
China mwaka 1992, na ilitenga
fedha nyingi kuanzisha vitengo
vyake vya utafiti vya ngazi
ya kimataifa, vikiwa ni pamoja
na kituo cha utafiti cha Microsoft
nchini China, taasisi ya utafiti
ya Microsoft katika Asia na
kituo cha teknolojia cha Microsoft
duniani, na kuifanya kampuni
ya Microsoft nchini China
kuwa tawi lake lenye uwezo
mkubwa duniani.
Hadi hivi sasa, Kampuni ya
Microsoft imejenga viwanda
viwili vya ubia nchini China.
Kampuni hiyo ikiwekeza Yuan
za Renminbi milioni 19, ilianzisha
Kampuni ya Software ya Zhongguancun
kwa ubia na Kampuni ya Sitong,
na kuanzisha Kampuni ya Softwere
ya Weichuang ya Shanghai kwa
kufanya ubia na Kampuni ya
Uwekezaji ya Lianhe ya Shanghai.
Aidha, Kampuni ya Microsoft
imeingia ubia pamoja na Chuo
Kikuu cha Mawasiliano cha
Shanghai, Kampuni ya Uwekezaji
ya Lianhe ya Shanghai na Kampuni
ya Soft Weare ya Pudong, Shanghai,
kuanzisha Chuo cha Softwere
cha Chuo Kikuu cha Mawasiliano
cha Shanghai na Kampuni ya
huduma ya sayansi na teknolojia
ya Chuo Kikuu cha Mawasiliano
cha Shanghai. Kampuni ya Microsoft
kwa jumla iliwekeza Yuan za
Renminbi milioni 4, zikichukua
10% ya mitaji yote iliyowekezwa.
Mbali na hayo, Kampuni ya
Microsoft imehamisha uzalishaji
wa X-box, ambazo ni bidhaa
zinazopendwa na watu wengi,
hapa China. Pia imeweka uzalishaji
wa mouse huko Guangdong, ambao
thamani ya uzalishaji imezidi
dola za kimarekani milioni
100 kwa mwaka.
|