|
|
|
|
|
|
|
中国国际广播电台
Shughuli za bima baada ya kuzorota
kwa miaka 29, zilianza kurejea
katika hali ya zamani toka mwaka
1980. Mwaka 1981, Shirika la
Bima la China, ambalo hapo zamani
ilikuwa idara moja ya serikali,
lilianzisha matawi yake kutoka
mikoa na miji inayodhibitiwa
moja kwa moja na serikali kuu
hadi wilaya. Kampuni za bima
zinazojulikana kwa Usalama na
Pasifiki, ambazo shughuli zake
hasa ziko katika sehemu ya pwani
ya China, zilianzishwa mwaka
1988. Mwaka 1996, Shirika la
Bima la China lilipiga hatua
moja kubwa katika kubadilisha
utaratibu wa usimamizi na uendeshaji
wa kazi, na kuungana na masoko
ya kimataifa. Kuanziashwa kwa
“Sheria ya bima” mwaka 1985
na kuanzishwa kwa kamati ya
usimamizi wa shughuli za bima
ya China mwaka 1988, kumeweka
mujibu wa sheria na kanuni za
uendeshaji kazi kwa shughuli
za bima nchini.
Hivi sasa, hapa nchini kuna
kampuni za bima na wakala wa
bima zaidi ya elfu 70, ambazo
zimeanzishwa bima za uzeeni,
afya, ajali na mali. Hivi sasa
kuna kampuni za bima za kigeni
zaidi ya 30 nchini China, wakati
kampuni zaidi ya 100 za nchi
za nje zimefungua ofisi zake
nchini, zikitarajia kuingia
katika soko la bima ya China.
Katika mwaka 2003, pato la kampuni
za bima za nchi za nje nchini
China lilikuwa Yuan zaidi ya
bilioni 388, likiwa ni ongezeko
la 27.1%.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|