Fedha za Renminbi na Usimamizi wa Fedha za Kigeni

中国国际广播电台


     
Fedha za Renminbi ni fedha za China zilizothibitishwa kisheria, ambazo zinatolewa na kusimamizwa na Benki ya Umma ya China. Kiasi cha kubadilisha fedha za Renminbi kwa fedha za kigeni, kinathibitishwa na Benki ya Umma ya China, na kutangazwa na idara ya usimamizi wa fedha za kigeni ya taifa. Ubadiliishaji wa fedha za Renminbi kwa fedha za kigeni, unadhibitiwa na serikali, na kutekelezwa na idara ya usimamizi wa fedha za kigeni ya taifa.
Mwaka 1994, China ilifanya mageuzi ya utaratibu wa fedha za kigeni, kufanya ubadilishaji wa fedha za Renminbi kwa fedha za kigeni kulingana na utaratibu wa kimataifa, ubadilishaji wa fedha za Renminbi na fedha za kigeni unashughulikiwa na benki na kuwa na utaratibu wa aina moja kwa shughuli za benki za China katika masoko ya fedha za kigeni. Kutokana na msingi huo, mwaka 1996 China iliweka mauzo ya fedha za kigeni ya kampuni au viwanda vilivyowekezwa na wafanyabiashara wa nchi za nje katika utaratibu wa shughuli za benki, na kutangulia kukubali kabla ya muda, kifungu cha nane cha mkataba wa Shirika la Sarafu Duniani kuhusu matumizi muhimu ya fedha za Renminbi yanaweza kubadilishwa kwa fedha za kigeni. Licha ya hayo, China imeshiriki na kukuza ushirikiano wa mambo ya fedha wa ubadilishanaji wa fedha wa pande mbili kati ya nchi za umoja wa Asia ya Kusini Mashariki na Japan na Korea ya Kusini. Hususan katika kipindi wakati mgogoro fedha wa Asia ulipozuka, si kama tu China ilishikilia kutopunguza thamani ya fedha za Renminbi, bali pia ilitoa misaada ya fedha kwa nchi zilizokumbwa na mgogoro ya fedha, na kuwa nguzo muhimu iliyohifadhi utulivu wa masoko ya fedha ya Asia.
Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2003, akiba ya fedha za kigeni ya China ilifikia dola za kimarekani bilioni 403.3, kiasi hiki ni ongezeko la dola za kimarekani bilioni 116.8 kulimo kile cha mwishoni mwa mwaka uliotangulia. Kiasi cha ubadilishaji kati ya fedha za Renminbi na fedha za kigeni kinatulia kinadumishwa katika hali ya utulivu.