|
|
|
|
|
Pato na Matumizi ya Wakazi
|
|
中国国际广播电台
Ikiulinganishwa na miaka zaidi
ya 50 iliyopita, kiwango cha
maisha ya watu wa China kimeinuka
sana, na hata ikilinganishwa
na kile cha miaka zaidi ya 20
iliyopita, kimeinuka kwa udhahiri.
Pato la watu linaongezeka kwa
mfululizo, na mali zao pia zimeongezeka.
Hivi sasa watu wa China wanatumia
fedha zaidi katika kununua nyumba,
magari, kompyuta, vyeti vya
hisa na kwenda kutembelea nchi
za nje.
Katika kipindi cha miaka zaidi
ya 20 baada ya mwaka 1979, uchumi
wa China ulipata maendeleo ya
kasi, na pato la wakazi pia
liliongezeka kwa haraka. Takwimu
zilizokusanywa zinaonesha kuwa
wastani wa pato la wakazi wa
sehemu za vijijini kwa mwaka
2002 ulifikia Yuan 2,476 kutoka
Yuan 134 mwaka 1978, na wastani
wa ongezeko la pato ulikuwa
7.2% kwa mwaka. Wastani wa pato
la wakazi wa mijini ulifikia
Yuan 7,703 kutoka Yuan 343,
ambalo ni ongezeko la 6.7% kwa
mwaka.
Mwaka 2003, maisha ya wakazi
wa China yaliendelea kuboreshwa.
Wastani wa pato la wakazi wa
mijini ulikuwa Yuan 8,472. Na
baada ya kuondoa mfumuko wa
bei, ongezeko halisi lilikuwa
9%, wastani wa pato la wakazi
wa vijijini ulikuwa Yuan 2,622
likiwa ni ongezeko la 4.3%,
ambapo fedha za matumizi ya
vyakula zilichukua 37.1% ya
jumla ya matumizi ya fedha kwa
wakazi wa mijini ambalo ni pungufu
kwa 0.6%, wakati zile za wakazi
wa vijijini zilikuwa 45.6%,
ambalo ni pungufu kwa 0.6% pia.
Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka
jana magari ya binafsi yalifikia
milioni 4.89, likiwa ni ongezeko
la magari milioni 1.46 kuliko
yale ya mwaka uliotangulia.
Hivi sasa hali ya upungufu wa
chakula na bidhaa zinazohitajika
kwa matumizi ya kila siku, imetoweka
kabisa. Mabadiliko ya matumizi
ya fedha kwa wakazi yanaonesha
kuwa fedha zinazotumika kununua
chakula, nguo na mahitaji ya
lazima zimepungua, lakini fedha
zinazotumika katika kujiendeleza
na kununua vitu vinavyoboresha
maisha, kama vile nyumba, magari,
simu za mikononi, matibabu na
utunzaji wa afya, zinaongezeka
haraka, na maisha ya wakazi
yanaboreshwa hatua kwa hatua.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|