中国国际广播电台
BIMA YA UZEENI
Katika miaka ya karibuni, bima
ya uzeeni imekuwa ikiendelea
kukua kwa haraka. Zamani bima
hiyo iliwahusu wafanyakazi wa
viwanda vya kserikali na ushirikika,
lakini hivi sasa imekuzwa hadi
kwa wafanyakazi wa viwanda vyote
na idara zisizo za uzalishaji
mali ambazo zinaendeshwa kama
za uzalishaji wa mali. Hivi
sasa haki za wafanyakazi wa
viwanda visivyo vya kiserikali
pia zimehakikishwa. Hadi mwishoni
mwa mwaka 2002, nchini China
kulikuwa na wafanyakazi milioni
111.29, na wastafu milioni 36.08,
ambao walishiriki bima ya uzeeni.
Na ilipofika mwishoni mwa mwaka
2003, idadi ya watu walioshiriki
kwenye bima ya uzeeni ilikuwa
milioni 154.90, likiwa ni ongezeko
la milioni 7.53.
BIMA AFYA
Bima ya afya kimisingi imefikia
viwanda na idara zote zisizo
za uzalishaji wa mali, ofisi
za serikali na makundi katika
jamii ya mijini. Bima ya aina
hiyo ni moja ya bima za jamii
inayoendelezwa katika maeneo
makubwa. Katika mwaka 2002,
idadi ya hospitali, zahanati
na vituo vya kuzuia maambukizi
ya maradhi nchini China ilifikia
laki 2.9, vitanda vya wagonjwa
milioni 3.21, pamoja na madakatari
na wauguzi milioni 4.44. Katika
miji mikubwa kama ile ya Beijing,
Shanghai, Tianjin na Chongqing,
kuna hospitani za hali ya
juu za kansa, ugonjwa na moyo
na mishipa ya damu, macho,
meno, tiba za jadi ya China,
maradhi ya kuambukiza, hospitali
maalumu za aina mbalimbali.
Katika miji ya wastani ya
mikoa, kuna hospitali zenye
zana za kisasa na hospitali
maalumu. Hivi sasa, katika
sehemu ya vijijini kuna mfumo
wa utibabu wa ngazi za wilaya,
tarafa na vijiji. China ina
hozpitali za ngazi ya wilaya
zaidi ya 2,000 pamoja na zahanati
elfu 48 za tarafa.
Katika mwisho wa mwaka 2003,
idadi ya watu walioshiriki
bima ya utibabu ilikuwa milioni
108.95, likiwa ni ongezeko
la milioni 14.94, ambao milioni
79.77 ni wafanya kazi, na
milioni 29.18 ni wastafu kazi.
BIMA YA KUKOSA AJIRA
China ni nchi yenye idadi
kubwa ya watu, hivyo inakabiliwa
shinikizo kubwa la ajira.
Ili kupunguza tatizo la ajira,
toka mwaka 1993, serikali
ya China ilitekeleza sera
za soko la nguvu-kazi, kutafuta
njia za kuongeza ajira. Serikali
ya China ilianzisha mradi
wa kuwapatia kazi wafanyakazi
waliopunguzwa kutoka viwanda
vya kiserikali kutokana na
marekebisho ya muundo wa uzalishaji
mali. Hadi mwishoni mwa mwaka
2002, idadi ya watu wenye
ajira katika miji yote nchini
ilikuwa milioni 247.80,. Toka
mwaka 1998, zaidi ya wafanyakazi
milioni 18 waliopunguzwa kutoka
kwenye viwanda vya serikali,
walipata ajira mpya kwa njia
za mbalimbali. Mwishoni mwa
mwaka 2002, idadi ya watu
waliokosa ajira ilikuwa kiasi
cha 4%. Kufuata utaratibu
wa bima ya kukosa ajira katika
idara mbalimbali zisizo za
uzalishaji mali, kumehimiza
uhamiaji mwafaka wa nguvukazi
na kuanzishwa kwa soko la
nguvukazi. Ilipofika mwishoni
mwa mwaka 2003, idadi ya watu
walioshiriki kwenye bima ya
kukosa ajira nchini China
ilikuwa milioni 103.73. Miji
yote nchini ikiwa ni pamoja
ya ngazi ya wilaya, imefuata
utaratibu wa dhamana ya kiwango
cha chini cha maisha, ambao
unatoa dhama ya maisha ya
kiwango cha chini kwa wakazi
wa mijini ambao pato lao ni
chini ya kiwango cha chini
katika miji wanayoishi. Mwaka
2003, wakazi milioni 22.35
wa mijini walipata dhamana
ya maisha ya kiwango cha chini.
Hivi sasa utaratibu huo umetatua
shida ya wakazi maskini wa
miji ya China.
|