中国国际广播电台
Mto Changjiang una rasimali
kubwa ya maji, mradi wa maji
wa Magenge Matatu ni mradi muhimu
wa kupunguza tatizo la maji
na kustawisha mto Changjiang.
Mradi wa Magenge Matatu uko
katika sehemu ya Sandouping,
ya mji wa Yichang, mkoa wa Hubei,
sehemu ya kati ya mto Changjiang.
Katika sehemu hiyo Mto Changjiang
ni mpana, chini yake kuna mawe
magumu na makubwa ya granite,
yanayoweza kudhibiti maji ya
sehemu ya juu ya mto yenye eneo
la kilomita za mraba 100, ambapo
maji yanayopita huko ni mita
za ujazo karibu bilioni 500
kwa mwaka.
Ujenzi wa mradi wa maji wa
Magenge Matatu unatumia mpango
wa kukamilishwa moja kwa moja,
kulimbikiza maji kwa viplindi
mbalimbali, na kuhamisha wakazi
hatua kwa hatua. Sehemu ya
juu ya ukingo wa maji ya bwawa
ina urefu wa mita 3,035, maji
baada ya kulimbikizwa katika
hali ya kawaida ni yanakuwa
na kina cha mita 175. Bwawa
la maji la mradi huo linaweza
kulimbikiza jumla ya mita
za ujazo bilioni 39.3.
Baada ya ujenzi wake kukamilika,
mradi wa Magenge Matatu utakuwa
na uwezo mkubwa wa kuzuia
mafuriko, kuzalisha umeme,
kuendeleza uchukuzi, ufugaji
samaki, utalii, kuhifadhi
mazingira ya asili, kuboresha
mazingira, kuhamisha wakazi
katika maeneo ya ustawishaji,
kupeleka maji kutoka sehemu
ya kusini kwenda sehemu ya
kaskazini na kumwagilia maji
mashamba.
|