Mradi wa Kupeleka Maji Kaskazini Kutoka Kusini

中国国际广播电台


     
Sehemu ya kusini ya China Ina maji mengi, lakini sehemu ya kaskazini ina upungufu wa maji. Ili kupeleka maji ya sehemu ya kusinii kwa sehemu ya kaskazini yenye ukame, wanasayansi na wahandisi wa China walifanya uchunguzi na upimaji porini kwa miaka 50.

Maji ya sehemu ya kusini yanapelekwa sehemu ya kaskazini kwa njia tatu za mashariki, kati na magharibi, ambazo zinakutana na mito minne mikubwa ya Changjiang, Manjano, Huai na Hai, ili kugawa rasilimali ya maji kufuatana na hali halisi.

Njia ya mashariki: kuchukua maji ya mto Changjiang katika mji wa Yangzhou, ulioko sehemu ya chini ya mto Changjiang, kupelekwa sehemu ya kaskazini kwa kupitia mfereji kati ya Beijing na Hangzhou na mito mingine inayokwenda sambamba nao, na kuungana na maziwa ya Hongze, Luoma, Nansi na Dongping. Maji yanayoletwa kutoka sehemu ya kusini yatapelekwa kwa njia mbili ndogo, ambazo moja ni inaelekea sehemu ya kaskazini kupitia mto Manjano; na njia nyingine inaelekea upande wa mashariki hadi Yantai na Weihai, mkoani Shandong.

 
 

 Njia ya katikati inachukua maji kutoka bwawa la maji la Danjiangkou, kuelekea sehemu ya kaskazini sambamba na njia ya reli kati ya Beijing na Guangzhou hadi miji ya Beijing na Tianjin.

Njia ya magharibi ni kuchukua maji kutoka bwawa la maji litakalojengwa karibu na mto Tongtian, tawi la mto Yalong na mto Dadu katika sehemu ya juu ya mto Changjiang, na kuyapeleka hadi sehemu ya juu ya mto Manjano. Uwezo wa kupeleka maji kwa njia hizo tatu ni mita za ujazo bilioni 44.8 katika mwaka 2050, ambazo njia ya mashariki ni mita za ujazo bilioni 14.8, njia ya kati ni bilioni 13 na ya magharibi ni mita za ujazo bilioni 17.

Ujenzi wa mradi huo wa kupeleka maji unafanywa kwa vipindi tofauti kufuatana na hali halisi. Hivi sasa ujenzi umeanza katika sehemu nne za njia za mashariki na kati.