Mradi wa Kupeleka Gesi

中国国际广播电台


    
Gesi ya sehemu ya magharibi inayotoka katika mikoa ya Xinjiang, Qinghai, Sichuan na ukanda wa Eerduosi, inatarajiwa kupelekwa sehemu ya mashariki ya delta ya mto Changjiang.

Sehemu za kati na magharibi za China kuna mabonde 6 yenye mafuta ya asili ya petroli na gesi, ambayo ni pamoja na Talimu, Zhengeer, Duha, Chaidamu, Eerduosi na Sichuan. Rasilimali za gesi zinakadiriwa kuwa ni mita za ujazo bilioni 2.24 na kuchukua 58.9% ya jumla ya rasilimali za gesi ya China, ambayo ni mita za ujazo trilioni 3.8. Kutokana na hali ya rasilimali za gesi, pamoja na uchunguzi na upimaji wa hivi sasa, serikali imeamua kuanzisha ujenzi wa mradi wa kupeleka gesi ya sehemu ya magharibi kwenye sehemu ya mashariki, kuharakisha ujenzi wa kutandika mabomba ya kupelekea gesi, licha ya kujenga njia ya mabomba ya kupelekea gesi kutoka mkoa wa Shanxi katika sehemu ya Beijing, zitajengwa njia 3 za kupelekea gesi ya asili kutoka Talimu kwenda Shanghai, kutoka Sebei ya mkoa wa Qinghai kwenda Xining na Lanzhou, na kutoka wilaya ya Zhong ya Chongqing kwenda mji wa Wuhan mkoani Hubei, ili kubadilisha hali bora ya rasilimali kuwa hali bora ya uchumi na kukidhi mahitaji ya haraka ya sehemu ya mashariki kwa gesi ya asili. Aidha, kutokana na mpango unaobuniwa hivi sasa, mabomba ya kupelekea ges kutoka Seberia ya magharibi ya Russia, yataungana na mabomba makubwa ya kupeleka gesi ya mradi wa kupeleka gesi ya sehemu ya magharibi kwa sehemu ya mashariki. Mbali na hayo, mpango mwingine unabuniwa hivi sasa wa kuchukua gesi ya Seberia ya mashariki ya Russia, nchi hizo pia zinahesabiwa kama ni kupeleka gesi ya sehemu ya magharibi katika sehemu ya mashariki.

Kwa namna nyingine, kupeleka gesi ya sehemu ya magharibi katika sehemu ya mashariki ni mradi wa kupeleka gesi kutoka sehemu ya Talimu ya mkoa wa Xinjiang katika delta ya mto Changjiang ya Shanghai. Njia hiyo ya mabomba, ambayo ina urefu wa kilomita 4,200, na mabomba yenye mpenyo milimita 1118, inapitia mikoa 8 ikiwemo Xinjiang, Jiangsu na mji wa Shanghai, uwezo wake wa kupeleka gesi ni mita za ujazo bilioni 12, na kugharimiwa Yuan bilioni 120.

Hivi sasa, ujenzi wa mradi wa kupeleka gesi umekamilishwa kwa 48%, na ujenzi wa sehemu ya mashariki ya njia ya mabomba umekamilika kabisa, na kuanza kupeleka gesi ya asili sehemu ya mashariki ya China.