Mradi wa Kupeleka Umeme

中国国际广播电台


     
Mradi wa kupeleka umeme kutoka sehemu ya magharibi kwenda sehemu ya mashariki ni mradi kwa ajili ya kupeleka umeme mwingi kutoka sehemu ya magharibi kwenda sehemu iliyoendelea ya mashariki. Kwa kuwa sehemu nyingi za uzalishaji wa umeme ziko katika sehemu za magharibi na kaskazini, lakini matumizi ya nishati ya umeme yako katika sehemu zilizoendelea za kandokando ya reli kati ya Beijing na Guangzhou na upande wa mashariki ya njia hiyo ya reli.

Mradi wa kupeleka umeme wa magharibi katika sehemu ya mashariki ni wa kujenga njia tatu za kupleleka umeme za kaskazini, katikati na kusini.

Njia ya kaskazini ni pamoja na mifumo ya umeme ya kaskazini mashariki, kaskazini , Shandong na kaskazini magharibi, hususan kuzalisha umeme kwa nguvu za maji katika sehemu ya kaskazini magharibi na kupeleka umeme kwa mifumo ya umeme ya Beijing, Tianjin,Hebei na Shandong.

Njia ya katikati ni pamoja na mifumo ya umeme ya sehemu za mashariki, katikati, Sichuan, na Fujian, hususan kuzalisha umeme kwa nguvu za maji ya mto Changjiang, na kupeleka umeme kwa sehemu za katikati, mashariki na Fujian, ambazo ni sehemu kubwa ya kupelekwa umeme kutoka sehemu ya magharibi, na kuleta athari kubwa kwa mfumo wa umeme wa nchi nzima.

Njia ya kusini ya kupeleka umeme ni kuzalisha umeme kwa nguvu za maji za mto Wu ulioko mkoani Guizhou, mto Lancang na mto mwekundu ulioko mkoani Yunnan, pamoja na umeme unaozalishwa na kiwanda cha umeme cha Kengkou cha mikoa miwili ya Yunnan na Guizhou na kupeleka umeme kwenye sehemu za mkoa wa Guangdong. Mradi wa kupeleka umeme kutoka sehemu ya magharibi katika sehemu ya mashariki ni mradi mkubwa nchini China, na ni sehemu muhimu ya mkakati uliotolewa na serikali ya China wa kustawisha sehemu ya magharibi, ambayo inaunganisha rasilimali nyingi za sehemu ya magharibi na masoko makubwa ya sehemu ya mashariki, na itachangia maendeleo makubwa ya sekta ya uzalishaji wa umeme na uchumi wa taifa.