中国国际广播电台
Kituo cha viwanda cha zamani
cha sehemu ya kaskazini mashariki
ya China kilikuwa muhimu sana
kwa uchumi wa taifa na maendeleo
ya jamii. Mwanzoni mwa kipindi
cha uchumi wa mpango, uzalishaji
wa mitambo na sekta ya uzalishaji
wa chuma na chuma cha pua, ilitoa
mchango mkubwa kwa ujenzi wa
uchumi wa China. Lakini, kwa
kuwa kituo cha viwanda vya sehemu
ya kaskazini mashariki kiliundwa
miaka mingi iliyopita, hivi
sasa baadhi ya sekta za uzalishaji
mali zimeingia katika kipindi
cha kuzorota. Nguvu zake za
ushindani zimepungua, lakini
sekta mpya za kuzibadilisha
bado hazijaimarika, hususan
baadhi ya miji yenye rasilimali
inakabiliwa na matatizo mengi.
Kuhusu matatizo hayo, serikali
ya China imeamua kuharakisha
marekebisho, mageuzi na ustawishaji
wa kituo cha viwanda cha zamani
cha sehemu ya kaskazini mashariki.
Kwa kukariri maneno ya waziri
mkuu wa China Bw. Wen Jiabao,
ustawishaji wa kituo cha zamani
cha viwanda cha sehemu ya
kaskazini mashariki, utarekebisha
muundo wa uchumi, ambao ni
pamoja na kurekebisha muundo
wa sekta ya uzaliishaji mali,
muundo wa utaratibu wa umilikaji
wa vyombo vya uzalishaji mali
na muundo wa uchumi wa taifa.
Hii ni miongozo muhimu katika
kustawisha kituo cha viwanda
cha zamani. Kuhimiza mageuzi
ya kiteknolojia katika viwanda
ni shughuli muhimu. Kuleta
maendeleo ya pande zote yenye
uwiano na endelevu ni sera
za muda mrefu; Kukamilisha
ujenzi wa mfumo wa ajira na
dhamana ya jamii ni dhana
kwa ustawishaji wa kituo hicho
cha zamani; na Kuharakisha
maendeleo ya sayansi, teknolojia
na elimu ni matakwa muhimu
ya ustawishaji wa viwanda
vya zamani vya sehemu ya kaskazini
mashariki ya China.
Hivi sasa, serikali ya China
inaandaa sera ya mpango wa
marekebisho ya kituo cha viwanda
cha zamani cha sehemu hiyo,
mikoa mitatu ya sehemu ya
kaskazini mashariki nayo inafanya
utafiti ili kubuni mpango
wa marekebisho na mageuzi
wa sehemu hiyo.
|