Uhusiano Kati ya China na Russia

中国国际广播电台

   

 

Tarehe 2 Oktoba, 1949, China na Urusi ziliwekeana uhusiano wa kibalozi. Mwezi Agosti, 1991, Shirikisho la Urusi lilisamblatika, tarehe 27 Desemba mwaka huo, China na Russia zilisaini kumbukumbu ya mazungumzo na kuondoa uhusiano wa kibalozi kati ya China na Urusi ya zamani. Mwaka 2001, uhusiano wa kiwenzi na kimkakati kati ya China na Russia ulifikia kiwango kipya, ambapo uaminifu wa kisiasa kati ya pande hizo mbili uliongezeka, na mawasiliano kati ya viongozi wakuu yamezidi kuwa barabara zaidi. Rais Jiang Zemin na rais Vladimir Putin walikutana mara tatu mwaka huo, na kuongea kwa simu mara 6. Mkataba wa ujirani mwema, urafiki na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili uliosainiwa mwaka 2001 pamoja na taarifa ya pamoja iliyotolewa mwaka huo zilithibitisha kwa njia ya kisheria wazo la amani la kuweka urafiki vizazi hadi vizazi, na daima kutofanya uhasama kati ya nchi hizo mbili na wananchi wa nchi hizo mbili.

Tarehe 26 hadi 28 Mei, 2003, rais Hu Jintao wa China alifanya ziara nchini Russia.

Katika maika ya hivi karibuni, uhusiano wa kiuchumi na kibiashara na ushirikiano wa kiuchumi na kiteknolojia kati ya nchi hizo mbili umeimarishwa siku hadi siku. Nchi hizo mbili zimeongeza zaidi siku hadi siku mawasiliano na ushirikiano katika sekta za utamaduni, sayansi na teknolojia na elimu. Na vikundi vya nyimbo na ngoma vya China na Russia vimetembeleana na kufanya maonesho mara kwa mara.

Kuhusu suala la mipaka. Mpaka kati ya China na Russia una urefu wa kilomita 4370 . Kuna tatizo la mipaka lililobaki katika historia kati ya nchi hizo mbili. Nchi hizo mbili zikifuata mkataba wa hivi sasa kuhusu mipaka ya nchi hizo mbili, na kufuata kanuni za sheria ya kimataifa zilizotambuliwa duniani, zimefanya mazungumzo ya miaka mingi, kushauriana kwa usawa, kuelewana na kulegeza masharti, zikathibitisha mwelekeo wa 97 % ya mstari wa mipaka.

Hivi sasa bado haujathibitisha mwelekeo wa mstari wa mpaka wa sehemu mbili za Kisiwa cha Heixiazi na Abageituzhouzhu zilizoko mashariki ya mpaka kati ya China na Russia, pande hizo mbili zitafuata kanuni ya haki na usawa, kuelewana na kurudi nyuma, kutatua haraka iwezekanavyo tatizo la mipaka lililobaki.