Chen Yi

中国国际广播电台


Chen Yi: Alikuwa mmoja kati ya waanzilishi na viongozi wa Jeshi la ukombozi wa umma la China, ambaye pia ni mtaalamu wa kijeshi na jenerali mkuu wa Jamhuri ya watu wa China. Baada ya kuzaliwa kwa China mpya, aliwahi kuwa naibu waziri mkuu, waziri wa mambo ya nje na naibu mwenyekiti wa kamati kuu ya kijeshi.

Kuanzia mwaka 1958 akiwa naibu waziri mkuu na waziri wa mambo ya nje, alifanya juhudi kubwa kutekeleza sera na fikra za kidiplomasia Mao Zedong na Zhou Enlai, kushiriki katika utungaji wa mikakati na sera za kidiplomasia za China mpya, kumsaidia Zhou Enlai kushiriki shughuli nyingi muhimu za kidiplomasia.