Qiao Guanhua

中国国际广播电台


Qiao Guanhua: Alikuwa waziri wa mambo ya nje wa China toka mwaka 1974 hadi 1976.

Alizaliwa huko Yancheng mkoani Jiangsu. Aliwahi kusoma nchini Ujerumani na alipata shahada ya tatu ya falsafa. Wakati wa kupambana na uvamizi wa Japan, alishughulikia kazi za habari na kuandika makala za maelezo kuhusu habari za kimataifa. Baada ya kuzaliwa kwa Jamhuri ya watu wa China, alikuwa naibu mkurugenzi wa kamati ya sera ya kidiplomasia katika wizara ya mambo ya nje ya China, msaidizi wa waziri wa mambo ya nje, na naibu waziri wa mambo ya nje. Katika shughuli zake za kawaida, alitunga mara kwa mara au kuandika nyaraka muhimu za mambo ya kidipolomasia.