Qian Qichen

中国国际广播电台


Qian Qichen : Alikuwa waziri wa mambo ya nje wa China toka mwaka 1988 hadi 1998.

Alizaliwa Mwezi Januari, 1928, huko Jiading, Shanghai. Toka mwaka 1972 hadi 1982, alikuwa balozi mdogo wa China nchini Urusi ya zamani, balozi wa China nchini Guinea, mkurugenzi wa idara ya habari katika wizara ya mambo ya nje ya China. Kuanzia mwaka 1988, alikuwa waziri wa mambo ya nje, katibu wa kamati ya chama na mjumbe wa taifa. Kuanzia mwaka 1993 alikuwa mjumbe wa ofisi ya siasa ya kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha China, naibu waziri mkuu na waziri wa mambo ya nje wa China.