Li Zhaoxing

中国国际广播电台


Li Zhaoxing : Amekuwa waziri wa mambo ya nje wa China kuanzia mwaka 2003 mpaka sasa.

Alizaliwa Mwezi Oktoba, 1940 mkoani Shangdong, alihitimu masomo katika chuo kikuu cha Beijing mwaka 1964. Aliwahi kufanya kazi katika ubalozi wa China nchini Kenya. Alikuwa naibu mkurugenzi na mkurugenzi wa idara ya habari katika wizara ya mambo ya nje na msemaji wa wizara hiyo toka mwaka 1985 hadi 1990. Alikuwa mwakilishi wa kudumu wa China katika Umoja wa Mataifa toka mwaka 1993 hadi 1995. Alikuwa balozi wa China nchini Marekani toka mwaka 1998 hadi 2001. Alikuwa naibu waziri wa mambo ya nje toka mwaka 2001 hadi 2003. Mwezi Machi, 2003 alichaguliwa kuwa waziri wa mambo ya nje wa China.